Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Sunday, December 13, 2015

KADUTU: “NITASIMAMIA UBORESHAJI WA MAKUMBUSHO YA MTEMI MILAMBO”




Na Paul Christian, Ulyankulu.

Mbunge wa Jimbo la Ulyankulu wilaya ya Kaliua mkoani Tabora Mheshimiwa John Peter Kadutu ameahidi kuboresha mazingira ya makumbusho ya Mtemi Milambo yaliyopo katika eneo la Ikonongo.

Akizungumza mbele ya familia ya Mtemi Milambo mbunge huyo alisema viongozi wengi wamekuwa wakiahidi kuboresha mazingira ya Makumbusho hayo lakini wameshindwa kufanya hivyo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo mambo ya kisiasa.

Kadutu alibainisha kuwa eneo hilo la Makumbusho linapaswa kuboreshwa ili lilingane na hadhi ya Mtemi Milambo tofauti na ilivyosasa eneo hilo haliendani na heshima ya Mtemi huyo maarufu.

Aidha alizitaka serikali kuu na halmashauri ya wilaya ya Kaliua zianze kutambua na kuona umuhimu wa kuwaenzi watemi mbalimbali ambao waliongoza mapambano ya kupinga ukoloni.

Mbunge huyo alitoa wito kwa wadau mbalimbali kuungana kwa pamoja ili kutimiza azma ya kuboresha mazingira yanayozunguka Makumbusho ya Mtemi Milambo pamoja na watemi wengine waliomtangulia.

Mheshimiwa Kadutu alianisha baadhi ya faida zitakazojitokeza baada ya kuliboresha eneo hilo kuwa ni kuwavutia wageni wengi zaid wa ndani na nje ya Tanzania kufanya utalii ambao utakuza uchumi na kutoa ajira kwa wakazi wa jimbo la Ulyankulu.

Awali akisoma taarifa ya Makumbusho hayo afisa tarafa wa tarafa ya Ulyankulu John Chitanda alisema jamii inayoishi kuzunguka makumbusho hayo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa shule, zahanati, barabara na visima virefu vya maji.

Eneo la Makumbusho ya Mtemi Milambo lipo katika eneo la kijiji cha Usigala barabara ya 44 katika jimbo la Ulyankulu na mtemi huyo alifariki mwaka 1884.

No comments: