Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Monday, December 14, 2015

LIGI DARAJA LA PILI NGAZI YA TAIFA YAENDELEA KATIKA UWANJA WA ALLY HASSAN MWINYI.



Na Ramadhan Faraji, Tabora.

Timu ya Abajalo yenye masikani yake wilaya ya Igunga mkoani Tabora imeshindwa kuutumia vyema uwanja wa nyumbani wa Ally Hassan Mwinyi baada ya kukubali kichapo cha magoli 3 kwa 1 kutoka kwa Singida United ya mjini Singida.

Mechi hiyo ambayo ilichezwa Jumapili na kushindwa kumalizika ndani ya dk. 90 kutokana na mvua kubwa iliyonyesha mjini Tabora,kabla ya  mwamuzi wa kati kuiahirisha mechi hiyo Singida United walikuwa wakiongoza kwa mabao 2 kwa 1.

Mechi hiyo iliendelea tena Jumatatu asubuhi kwa timu hizo kumalizia dk. 22 zilizosalia kabla ya mechi hiyo kuhairishwa siku ya Jumapili ambapo Singida United waliweza kuzitumia vyema dk hizo 22 kwa kufunga goli moja na kufanya matokeo kusomeka mabao 3 kwa 1 hadi dakika 90 za mchezo zinakamilika.

Aidha Ligi Daraja la Pili  ngazi ya Taifa imeendelea tena jioni ya siku ya Jumatatu katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi kwa kuzikutanisha timu za Milambo FC ya Tabora na Mvuvuma ya Kigoma.

Shukurani zimwendee mchezaji wa Milambo FC Rashid Kabole aliyeipatia timu yake goli moja la pekee na la ushindi kufuatia kuukwamisha nyavuni mpira wa penati.

Hadi mwisho Milambo FC  watoto wa Nyumbani waliibuka na Ushindi wa bao moja kwa sifuri dhidi ya wapinzani wao Mvuvuma FC na hivyo kujikusanyia pointi tatu muhimu.

No comments: