Na Hastin Liumba,Tabora
Hatimaye
Madiwani wa halmashauri ya Manispaa ya Tabora wamefanya uchaguzi wa
Meya na Naibu baada ya kuvutana kwa muda
mrefu.
Uchaguzi
huo uligubikwa na ubishani wa namna ya kupiga kura baada ya mkurugenzi mtendaji
wa Manispaa hiyo Zipola Liana kutoa maelekezo ya utaratibu wa kupiga kura
kwenye kizimba jambo lililopingwa na
baadhi ya madiwani waliotaka kupiga kura mahali walipokaa.
Hata
hivyo afisa wa uchunguzi mwandamizi wa TAKUKURU mkoa wa Tabora Henri Mwankusye alitoa
ufafanuzi wa sheria ya TAKUKURU pamoja na ile ya uchaguzi kwa madiwani hao.
Lakini
wakati afisa huyo wa TAKUKURU akitoa ufafanuzi wa vifungu vya sheria, baadhi ya
madiwani walikuwa wameanza zoezi la kupiga kura huku wakiwa wameketi katika
nafasi zao.
Kutokana na hali hiyo mbunge wa Tabora mjini Emmanuel Mwakasaka aliomba mwongozo na kutaka uchaguzi huo uanze upya kwa kuwa tayari dosari imejitokeza kwa baadhi ya madiwani kupiga kura huku wakioneshana.
“Ndugu zangu hapa tumepewa mwongozo na viongozi wetu na tayari kura 17 zimeshapigwa kimsingi tunapaswa tuanze upya kwa kufuata
mwongozo ili tusipate malalamiko ya dosari za uchaguzi huu.’Alisema
Mwakasaka.
Mabishano hayo yalidumu kwa takribani nusu ambapo madiwani waliridhia kupiga kura kwenye kizimba na kutumbukiza kura kwenye kisanduku.
Vyanzo vya taarifa vimebainisha kuwa baadhi ya madiwani
wa CCM walitaka kuvuruga uchaguzi huo kwa kumpigia mgombea wa CHADEMA Conel Ng`andu kwa sababu wagombe waliowaunga mkono kwenye nafasi ya Umeya kutopitishwa na vikao vya CCM.
Katika uchaguzi huo diwani wa kata ya Mpera Leopord Ulaya wa CCM
alishinda kwa kura 32 dhidi ya mgombea wa CHADEMA Conel Ng`andu wa kata ya Malolo aliyepata kura 8.
Kutokana na hali hiyo mbunge wa Tabora mjini Emmanuel Mwakasaka aliomba mwongozo na kutaka uchaguzi huo uanze upya kwa kuwa tayari dosari imejitokeza kwa baadhi ya madiwani kupiga kura huku wakioneshana.
“Ndugu zangu hapa tumepewa mwongozo na viongozi wetu na tayari kura 17 zimeshapigwa kimsingi tunapaswa tuanze upya kwa kufuata
mwongozo ili tusipate malalamiko ya dosari za uchaguzi huu.’Alisema
Mwakasaka.
Mabishano hayo yalidumu kwa takribani nusu ambapo madiwani waliridhia kupiga kura kwenye kizimba na kutumbukiza kura kwenye kisanduku.
Vyanzo vya taarifa vimebainisha kuwa baadhi ya madiwani
wa CCM walitaka kuvuruga uchaguzi huo kwa kumpigia mgombea wa CHADEMA Conel Ng`andu kwa sababu wagombe waliowaunga mkono kwenye nafasi ya Umeya kutopitishwa na vikao vya CCM.
Katika uchaguzi huo diwani wa kata ya Mpera Leopord Ulaya wa CCM
alishinda kwa kura 32 dhidi ya mgombea wa CHADEMA Conel Ng`andu wa kata ya Malolo aliyepata kura 8.
No comments:
Post a Comment