Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Monday, December 21, 2015

MARAIS WA FIFA NA SHIRIKISHO LA SOKA BARANI ULAYA WAMEFUNGIWA KUJISHIRIKISHA NA MASUALA YA MICHEZO KWA MIAKA MINANE.



Na Paul Christian.
 
Rais wa Shirikisho la Soka Duniani FIFA Sepp Blatter amesema yeye bado ni Rais wa shirikisho hilo licha ya kufungiwa kujihusisha na masuala ya michezo kwa muda wa miaka minane na kupigwa faini ya dola za kimarekani 50,000.

Kamati ya maadili ya shirikisho hilo imechukua hatua hiyo baada ya kubaini Blatter aliidhinisha malipo ya dola za kimarekani mil. 2 kwenda kwa Rais wa Shirikisho la Soka barani Ulaya UEFA Michel Platini mwaka 2011 ili asaidiwe kwenye uchaguzi uliofanyika mwaka huu.

Blatter amesema akiwa Rais wa shirikisho hilo hawajibishwi na kamati ya maadili ya FIFA isipokuwa mkutano mkuu wa shirikisho hilo ambao kwa mujibu wa ratiba umepangwa kufanyika mwezi Februari mwaka 2016.

Amesema, “ninaomba radhi, ninaomba radhi kwa ajili ya FIFA.”

Blatter amesikitishwa na utaratibu uliotumiwa wa kutoa taarifa za kufungiwa kwake kwa vyombo vya habari kabla ya kutaarifiwa yeye binafsi.

Aidha kamati hiyo ya maadili ya FIFA imemfungia Rais UEFA Michel Platini kutoshiriki masuala ya michezo kwa muda wa miaka minane kutokana na kupokea fedha hizo.

Sepp Blatter mwenye umri wa miaka 79 na ambaye amelitumikia shirikisho hilo kwa miaka 17 anatuhumiwa kwa kupokea hongo,rushwa, kutoa na kupokea zawadi mambo ambayo yako kinyume na maadili ya FIFA.

Hata hivyo uongozi wake ulikuwa unafikia ukomo mwezi Februari mwaka 2016 kufuatia kujiuzulu kwake mara baada ya kuchaguliwa mapema mwaka huu kutokana na tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa.





No comments: