NA Lucas Raphael,Urambo.
DEREVA wa
basi la Allys Star, Alfa Haji (37) lililopata ajali lilipokuwa likisafiri
kutoka wilaya ya Kaliua kuelekea jijini mwanza amefikishwa katika mahakama ya
hakimu mkazi wilaya ya Urambo mkoani Tabora akikabiliwa na mashitaka 22 ikiwemo
kusababisha vifo vya watu wanane na majeruhi 13.
Akisoma
mashitaka hayo mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo Hassani Momba
mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi mkaguzi msaidizi Felibet Pima alisema
kwamba mnamo desemba 15 mwaka huu majira ya saa 12 asubuhi katika kijiji cha
vumilia wilaya ya urambo mtuhumiwa huyo aliendesha gari kizembe na kupata ajali
iliyosababisha vifo vya watu wanane .
Alisema
kwamba licha ya kusababisha vifo vya watu wanane pia alisababisha majeruhi kwa watu 13.
Mwendesha
mashitaka huyo aliwataja marehemu waliotambuliwa kuwa ni Hamisi Ramadhani mkazi
wa Magiri mkoani Tabora,Grace Andrew(24) mkazi wa Ng'ambo Tabora, Paschal Abdul
(miezi 8) mkazi wa Bunda,Tipwege Kataga(20), Emeliana Tryphon(24) , Antoni
Julius Mkazi wa Wilayani Kaliua,Shija Anton mkazi wa Kaliua na Rahel Mussa
Mkazi wa Ulyankulu wilayani Kaliua.
Aidha
mwendasha mashitaka wa jeshi la polisi ,Pima aliwataja majeruhi mbele ya
mahakama hiyo kuwa ni Pili Juma (15),Maro Machano(50),Gift Mayunga(29),Ibrahimu
Hasani (25),Rahel Mabula (20)Jane Inosent(29) Anges Michael ,Godlifa Alois
(35).
Wengine
ni Santo Lufasiza (28) Mariamu Cosmas (38)Fatuma Juma (19) Yunge Sini (9) na
Marthar Luhende (21)
Hata hivyo mtuhumiwa huyo
alikana mashitaka yote 22 na amerudishwa rumande kwa usalama wake na kesi hiyo itatajwa
tena desemba 31 mwaka huu.
No comments:
Post a Comment