Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Wednesday, December 16, 2015

SAID KATALA:AWAPONGEZA WABUNGE WA MAJIMBO YA TABORA KASKAZINI NA IGALULA



Na Paul Christian, Tabora.

Wabunge wa majimbo ya Igalula Musa Ntimizi na Tabora Kaskazini Almas Maige wilayani Uyui mkoani Tabora wamepongezwa kwa namna wanavyotekeleza majukumu yao ndani ya CCM na kwa wananchi waliowachagua katika majimbo yao.

Pongezi hizo zimetolewa leo na Katibu wa Siasa, Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Uyui Bwana Said Katala wakati wa mahojiano maalum na mwandishi wa blog ya Tabora Watch.

Amesema wabunge hao wamesababisha watendaji na viongozi wa CCM ngazi ya mashina, matawi, kata na wilaya kutekeleza majukumu yao kwa ari na nguvu mpya baada ya kuwaunganisha kwa kuweka kando tofauti zilizojitokeza kwenye michakato ya uchuguzi uliopita.

Bwana Katala amebainisha kuwa wabunge hao kwa pamoja wameweza kuweka rekodi ambapo kwa mara ya kwanza katika historia ya chama wilayani humo wameitisha kikao cha kazi kilichowakutanisha wenyeviti na Makatibu wa CCM ngazi ya kata, Madiwani, wajumbe wa sekretariet ngazi ya wilaya pamoja na Kamati ya siasa ya wilaya hiyo.

Amesema kikao hicho kimewawezesha viongozi hao kuwa timu moja yenye lengo moja katika kuimarisha chama na kuisimamia serikali katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015.

Katibu huyo wa Siasa,Itikadi na Uenezi wa CCM wilaya ya Uyui amewataka wabunge hao kutokatishwa tamaa na watu wachache ambao wamekuwa wakitoa maneno ya uzushi kwa maslahi yao binafsi na kwamba wao wachape kazi tu.

Kikao hicho kilichoitwa “kikao cha kazi” kiliwahusisha viongozi hao kutoka kata 30 za majimbo ya Tabora Kaskazini na Igalula wilayani humo ambapo kwa pamoja walitoka na kauli mbiu ya "MAENDELEO KWANZA, MAJUNGU BAADAYE, HAPA KAZI TU."

No comments: