Na
Mwandishi Wetu,Kaliua
Wakiongea
kwenye kikao cha uchaguzi wa viongozi wa sungusungu wa kijiji cha hicho
wananchi hao walisema wamechoshwa na tabia ya polisi kuwatoza kiasi hicho cha
fedha kila yanapotokea mauaji ya ndugu zao.
Wakiongea
kwenye mkutano huo wananchi hao walisema yalitokea mauaji ya Nassor Ally na Juma
Mbogoni aliyeuawa Oktoba 7,2015 kwa shambulio la mapanga ndugu wa marehemu
walitozwa Tsh 600,000/= na polisi kama
gharama ya mafuta.
Wananchi
hao waliiomba serikali ya mkoa kuingilia kati kwani wamechoshwa na hali kuombwa
fedha hiyo huku wakilalamikia pia kila wanapofanya makosa ya kawaida hutozwa
hadi shilingi milioni nne.
Machemba
Ngeleja ambaye ni mwenyekiti wa kijiji cha Mwahalaja alisema yeye alisingiziwa
kosa la kula njama za kumdhuru mtendaji wa kijiji cha hicho Shukuru Ngoma
ambapo polisi walichukua magunia 20 ya mpunga na ng’ombe tisa.
Ngosai
Lutapia mkazi wa kijiji hicho alieleza kuwa alibambikiwa kesi ya bangi na kutozwa
faini ya Tsh 120,000/= na askari polisi
wa wilaya hiyo ya Kaliua.
Afisa
mtenda wa kijiji cha Mwahalaja Shukuru Ngoma akiongea kwenye mkutano huo alisema ni
kweli amekuwa akiwakamata watuhumiwa na kuwahifadhi ofisini kwake lakini siku moja wananchi walivunja mlango na kumuua
Juma Mbogoni na yeye aliwajulisha polisi na walipofika aliwakabidhi maiti hiyo.
Mtendaji
huyo alisema baadhi ya watu walikamatwa na polisi katika tukio hilo nikasikia
walitozwa fedha na kuachiwa huru lakini nashindwa kuthibitisha maana walikuwa
wakipelekwa Kaliua huku wengine wakitoa fedha kwa kujificha.
Ngoma
alisema kijiji chake kina kaya 455 na kwamba wakazi wake kwa sasa
wanaishi kwa hofu kwani wengi wao wamefilisika kwa kuuza ng`ombe ili watoe
fedha kwa polisi na kiwango kinachotozwa ni kati ya shilingi milioni moja hadi
tano kulingana na kosa analokutwa nalo.
Kuhusu
kuanzisha upya jeshi la sungusungu Ngoma alisema wameamua kufanya hivyo
kupunguza uhalifu kwani wananchi wamekuwa wakiishi kwa visasi vya ugoni na wizi
wa mali za watu.
Kamanda
wa polisi wilaya ya Kaliua (OCD) M R Markuhi alipoulizwa juu ya
malalamiko ya wananchi hao alisema hajui chochote wala hajapokea taarifa toka
kwa mwananchi ambaye aliombwa Tsh 600,000/= ya mafuta na kuahidi kulifanyia
uchunguzi suala hilo.
Kamanda wa
polisi mkoa wa Tabora (ACP) Khamis Seleman alisema hana taarifa hizo na kwamba
wananchi wanapaswa kuwataja askari wanaohusika na udanganyifu huo.
Alisema kama
kuna askari wamehusika atafanya uchunguzi wa kina na kuchukua hatua lakini pia
wananchi nao watoe ushirikiano kwani kiasi cha Tsh 600,000/= kwa madai za mafuta ni wizi.
No comments:
Post a Comment