Na Halima Ikunji ,Tabora.
Halmashauri
ya wilaya ya Uyui mkoani Tabora imevunja mkataba wa ujenzi wa jengo la wagonjwa
wa nje OPD katika hospitali ya wilaya hiyo kufuatia Mkandarasi kampuni ya SARAM
kukiuka masharti ya mkataba huo.
Akizungumza
na waandishi wa habari mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Hadija Makuwani
amesema kampuni hiyo ya jijini Dar es Salaam imesitisha shughuli za ujenzi wa
OPD hiyo iliyopo Isikizya makao makuu ya wilaya hiyo.
Amesema
mkandarasi huyo amesimamisha shughuli za ujenzi kwa muda wa miezi 9 na hivyo
kwenda kinyume na kifungu namba 62.2 cha mkataba huyo.
Hadija
ameeleza kuwa mkandarasi huyo pia alikiuka vifungu namba 10.1 na 10.2 vya
mkataba huo kwa kumtumia mtaalamu ambaye hatambuliki kwenye mkataba huo.
Mkurugenzi
huyo mtendaji ametaja sababu nyingine zilizosababisha kuvunjwa kwa mkataba huo
ni mkandarasi huyo kushindwa kuhudhuria vikao vya kazi vilivyoitishwa na
msimamizi wa mradi huo jambo ambalo ni kinyume na kifungu namba 35.2 cha
mkataba huo.
Hadija
amebainisha kuwa hatua za kuvunja mkataba huo zimezingatia kifungu cha 62.1
ambacho kinamtaka mwajiri au mkandarasi kuvunja mkataba endapo mmoja kati yao
atashindwa kutimiza masharti ya mkataba huo.
Aidha
amefanunua kuwa wakati mkataba unavunjwa mkandarasi huyo alikuwa ametekeleza
kazi yenye thamani ya sh. 138,109,468.86 na madai
anayostahili ni sh. 3,564,245.59 kama malipo ya kazi.
anayostahili ni sh. 3,564,245.59 kama malipo ya kazi.
Hadija
amekiri kuwa kiasi cha sh.5,650,157.95
kama malipo ya kinga iliyokuwa imekatwa kwenye hati alizokwishalipwa na kuongeza
kuwa malipo ya fedha hiyo atalipwa baada ya tathmini ya mwisho.
Mkurugenzi
huyo amebainisha kuwa gharama za mkataba wa kazi hiyo ilikuwa sh 299,654,364.60
huku nyongeza ikiwa ni sh 15,257,200.00 jambo linalofanya gharama ya mradi wote
kuwa kiasi cha sh 314,911,564.60.
“mkataba
huo umevunjwa rasmi tarehe 22 mwezi huu baada ya kujiridhisha pasipo shaka kuwa
mkandarasi ameshindwa kutimiza matakwa ya kisheria ya mkataba wake’, alisema Mkurugenzi.
No comments:
Post a Comment