Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Tuesday, February 16, 2016

ZAKARIA AICHANGIA MADAWATI 5 SHULE YA MSINGI ALIYOSOMEA MIAKA YA 1980, WEWE JE?



PICHA KUTOKA MAKTABA
Na Lucas Raphael, Nzega.

MDAU  wa elimu  Zakaria Luzwilo wa kata ya Puge wilaya ya Nzega Mkoani Tabora ametoa Msaada wa madawati 5 yenye thamani ya shilingi 300,000/-  kwa shule ya msingi Isunha kwa lengo la kukabiliana na upungufu wa madawati shuleni hapo.

Mdau huyo ambaye alisoma katika shule hiyo miaka 1980 amesema ametoa madawati hayo ili kuonyesha mchango wake pamoja na kuhamasisha watu wangine kujitolea kulikabili tatizo hilo. 
                                          
Akizungumza mara baada ya kukabidhi madawati hayo kwa mwalimu mkuu wa shule hiyo Mathew Shija, mdau huyo amesema  ametoa msaada huo  mdogo ili hamasa kwa watu wengine kujitolea hata kwa kidogo walichonacho kusaidia sekta ya elimu.

Zakaria amesema mwaka jana alialikwa na uongozi wa shule hiyo kuwa mgeni rasmi kwenye mahafali ya darasa la saba na kuhaidi kutoa msaada wa madawati hayo na kwamba ametimiza ahadi hiyo.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo ya msingi Shija amemshukuru mdau huyo wa elimu kwa msaada wa madawati hayo ambayo yatasaidia kupunguza pengo la mahitaji halisi ya madawati shuleni hapo.

Aidha amesema msaada huo ni mkubwa kutoka kwa mtu binafsi toka alipohamia shuleni hapo mwaka 2000.

Zakaria amempongeza mdau huyo wa elimu kwa kuonyesha moyo wa kizalendo na fadhila kwa shule aliyosomea. 

Mwalimu mkuu huyo amebainisha kuwa shule hiyo ina wanafunzi 355 na inakabiliwa na upungufu wa madawati 50 na yaliyopo ni sasa ni 100. 

No comments: