Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Sunday, February 7, 2016

SERIKALI YA KIJIJI YAKATALIWA, WANANCHI WAMUITA DC



Na Paul Christian, Tabora

Wananchi wa kijiji cha Ishihimulwa kata ya Bukumbi wilaya ya Uyui mkoani Tabora kwa mara nyingine wameikataa taarifa ya mapato na matumizi ya upangaji wa mnara wa simu za mkononi Airtel uliopo kwenye eneo la shule ya msingi Ishihimulwa kijijini humo.

Kwa kauli moja wananchi hao kupitia mkutano mkuu wa pili wa kijiji hicho walimzuia mtendaji wa kijiji hicho Jiji Numbu kuendelea kuisoma taarifa kuhusu mradi huo wa mnara wa simu kwa kuwa haikuakisi hali halisi ya mapato yanayolipwa na kampuni ya Airtel kwa uongozi wa shule hiyo.
Wananchi hao wamemshutumu mwalimu mkuu wa shule hiyo kutumia kwa manufaa yake binafsi fedha zinazotolewa kama malipo ya pango na kampuni inayomiliki mnara huo.

Msimamo huo wa wananchi umetolewa baada ya mara ya kwanza kuikataa taarifa ya mapato na matumizi ya mradi huo wa mnara wa simu iliyotolewa kwenye mkutano mkuu wa kijiji uliofanyika tarehe 18 mwezi uliopita na kuonyesha kuwa kwa mwaka wa 2015 mnara huo uliingiza mapato ya shilingi 90,000/= badala ya shilingi 1,600,000/= kwa mwaka kama ilivyoainishwa kwenye mkataba.

Aidha Katika mkutano huo wa pili wananchi hao waliikataa serikali ya kijiji inayoongozwa na Edward Daniel kwa kukaidi maagizo waliyopewa na diwani wa kata ya Bukumbi John Majala ya kuivunja kamati ya shule hiyo pamoja na kuwasilisha kwa wananchi hati ya benki inayoonesha mwenendo wa fedha wa akaunti ya shule husika.

Wananchi hao wamehoji mapato ya mnara huo wa simu  ili waweze kujenga choo cha wanafunzi wa shule hiyo ambao kwa sasa wanahangaika kwa kujihifadhi.

Aidha wamemshutumu mwalimu mkuu wa shule hiyo ya msingi kushindwa kuhudhuria mikutano mikuu ya kijiji kwa madai ya kuwa na majukumu ya kikazi hali inayoashiria kuna jambo analolificha kwa wananchi.

No comments: