Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Tuesday, February 9, 2016

MABONDIA WA TABORA WASHINDA KWA KNOCKOUT JIJINI DAR ES SALAAM



Na Deogratius Yagomba, Tabora.

Timu ya masumbwi (Ndondi) ya mkoani wa Tabora inayoshiriki kwenye michuano ya taifa imeendelea kufanya vizuri jijini Dar es Salaam.

Akiongea kwenye kipindi cha Meza ya michezo katibu na mwalimu wa kikosi hicho Yahaya Bageleza amewataja  mabondia  wanaowakilisha mkoa wa Tabora kwenye michuano hiyo kuwa ni  Bakari Athuman, Maneno Athuman, Musa Haruna  na Wami ramadhani.

Katibu huyo amebainisha kuwa mabondia walioshinda mapambano yao kwa knockout (KO) katika michuano hiyo ni Maneno Athuman na Musa Haruna.

Bageleza amesema bondia mmoja amepoteza pambano lake na mwingine anasubiri  ratiba ya pambano lake.


Hata hivyo ameulaumu uongozi wa serikali ya mkoa wa Tabora kwa kushindwa kuisaidia kifedha timu hiyo ambayo imekwenda kuwakilisha mkoa wa Tabora.


Hata hivyo Bageleza amewataka wapenda michezo na wadau kuisaidia timu hiyo ili iweze kufanya vizuri katika hatua nyingine ya michuano hiyo.

Akizungumza kwa njia ya simu mmoja wa mabondia hao Bakari Athumani amesema kuwa walilazimika kuuza baadhi ya vitu vyao ili kupata fedha za  kujikimu wakiwa safarini na kwenye mashindano hayo.

 

1 comment:

Unknown said...

Hivi mko wapi apa Tabora tujiunge na wengine