![]() |
WAZIRI WA ELIMU,SAYANSI,TEKNOLOJIA NA UFUNDI PROF. JOYCE NDALICHAKO |
NA Lucas Raphael, Kaliua.
Wanafunzi wapatao 700 wanakaa chini katika shule ya msingi Mtapenda iliyopo
Kata ya Ufukutwa wilayani Kaliua mkoani Tabora kutokana na kukosefu wa
madawati.
Licha ya ukosefu huo wa madawati shule hiyo inakabiliwa na changamoto nyingine ikiwemo ukosefu wa vyoo vya wanafunzi, upungufu wa vyumba vya madarasa, nyumba za walimu na walimu kutembea umbali wa zaidi ya kilomita 40 kwa siku.
Akizungumzia suala hilo diwani wa kata ya Ufukutwa Abdallah Hemeda amesema wanafunzi wa shule hiyo kwa sasa wanatumia choo chenye matundu manne ambacho kilikuwa cha walimu.
Licha ya ukosefu huo wa madawati shule hiyo inakabiliwa na changamoto nyingine ikiwemo ukosefu wa vyoo vya wanafunzi, upungufu wa vyumba vya madarasa, nyumba za walimu na walimu kutembea umbali wa zaidi ya kilomita 40 kwa siku.
Akizungumzia suala hilo diwani wa kata ya Ufukutwa Abdallah Hemeda amesema wanafunzi wa shule hiyo kwa sasa wanatumia choo chenye matundu manne ambacho kilikuwa cha walimu.
Amebainisha kuwa hali
hiyo imewafanya walimu wa shule hiyo kutumia choo kimoja kilichopo kwenye
nyumba moja ya mwalimu.
Diwani huyo ameiambia kamati ya Fedha na Mipango ya halmashauri ya wilaya ya Kaliua kuwa shule hiyo ina vyumba viwili vya madarasa na chumba kimoja kati ya hivyo hakijakamilika ujenzi wake.
Diwani huyo ameiambia kamati ya Fedha na Mipango ya halmashauri ya wilaya ya Kaliua kuwa shule hiyo ina vyumba viwili vya madarasa na chumba kimoja kati ya hivyo hakijakamilika ujenzi wake.
Abdallah amefafanua
kutokana na hali hiyo wanafunzi 700 wanalazimika kuvitumia vyumba hivyo vya
madarasa pamoja na kusomea chini ya miti ili kukidhi mahitaji.
Amebainisha kuwa hali
ya kufundisha na kujifunza huwa ngumu zaidi
wakati wa kipindi hiki cha mvua ambapo wanafunzi wote ulazimika
kujihifadhi kwenye vyumba hivyo vya madara huku walimu wakijihifadhi kwenye
nyumba ya mwalimu.
Ameongeza kuwa shule hiyo inakabiliwa
na mazingira magumu yanayowafanya walimu wake kuishi mjini na kulazimika kutembea
zaidi ya kilomita 40 kila siku.
Aidha diwani huyo amewapongeza walimu wa shule hiyo kwa kuifanya shule hiyo kuongoza kitaaluma kati ya shule za msingi zilizopo kwenye kata hiyo licha ya kukabiliwa na changamoto kadhaa. Mwalimu Mkuu msaidizi wa shule hiyo,Godfrey Alex ameitaka serikali kujenga vyumba vya madarasa, nyumba za walimu pamoja na miundombinu mingine kulingana na mahitaji ya shule. Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kaliua Haruna Kasele amesikitishwa na hali hiyo na kumtaka Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo kuhakikisha anajenga vyumba vya madarasa ili kuondoa tatizo la msongamano na kusomea chini ya miti. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Athuman Kihamia amesema agizo la mwenyekiti litaanza kutekelezwa ili kukabiliana na changamoto zinazoikabili hule hiyo. Amesema shule hiyo ni miongoni mwa zile ambazo hazikuwa katika utaratibu rasmi wa serikali kutokana na kujengwa na jamii ya wafugaji ambao wanahamahama. Mkurugenzi huyo amekiri kuanza kuzisaidia shule kama hizo ambazo ziko kwenye mazingira magumu ya kujifunzia na kufundishia. |
No comments:
Post a Comment