Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amekuwa akihimiza
wafanyabiashara kufanya biashara halali na kulipa kodi sahihi na kwa wakati.
Hatua
hiyo inalengo la kuongeza mapato ya serikali ili iweze kutimiza wajibu wake wa
kutoa huduma za kijamii, kugharamia miradi ya maendeleo pamoja na uendeshaji wa
serikali.
Rais
huyo wa awamu ya Tano ameonyesha nia ya dhati ya kubana matumizi ya
serikali,kuziba mianya ya ukwepaji kodi,kudhibiti matumizi mabaya ya madaraka na
kuifanya mifumo ya umma kufanya kazi yake ipasavyo.
Uchunguzi umebaini kuwa nia njema ya Rais Magufuli ya kuleta
uwiano wa kipato cha mwananchi wa kawaida na ukuaji wa uchumi wa nchi sanjari na kupunguza pengo
la kipato kati ya matajiri na masikini haiwezi kufanyikiwa pasipo kuwawezesha
wananchi kuwa sehemu ya mabadiliko husika.
Kwa upande wa wafanyabiashara ambao wanawajibika kulipa kodi
halali kwa serikali, ndio waajiri wakubwa wa Watanzania wenye elimu ya
chini,kati na hata elimu ya juu.
Kwa miaka mingi, wengi wa wafanyabiashara hao licha ya kujihusisha
na vitendo vya kuikosesha serikali mapato kwa kutokulipa kodi sahihi, wamekuwa
wakilipa mishahara duni wafanyakazi wao.
Kwa mantiki hiyo dhamira ya Rais Magufuli haiwezi kufanikiwa
endapo wafanyabiashara hao watalipa kodi stahiki kwa serikali, huku wakiendelea kulipa mishahara duni inayodhalilisha
utu wa mtanzania.
Tanzania imekuwa na udhaifu mkubwa wa kusimamia Sheria, Kanuni na Taratibu wakati wa kutimiza majukumu kwa maslahi ya umma na badala yake maslahi
ya wachache yamekuwa yakipewa nafasi hata kwa kupindisha Sheria.
Serikali
ya awamu ya Nne ilifanya jitihada za majadiliano, uundaji wa miundombinu na
usimamizi wa kisekta kwa lengo la kuboresha mishahara ya wafanyakazi katika
sekta binafsi.
Lakini hatua hiyo mara zote imeshindwa kufua dafu kwa
wafanyabiashara matajiri ambao wameonyesha kuwa na sauti zaidi ya Sheria, Kanuni na Taratibu za nchi.
Ushahidi wa kiburi, jeuri na dharau ya wafanyabiashara hao umejidhihirisha
kwa kugomea kuwapa mikataba wafanyakazi wao kwa madai na visingizio vilivyo nje
ya Sheria husika na serikali ikawa kimya.
Dkt. Magufuli atakapo kusanya kodi yake na kuacha wafanyakazi
wake wakiwa na usalama mdogo kwa kutokuwa na mikataba ya uhakika mbele ya
wafanyabiashara hao matajiri dhamira yake itashindwa kufikiwa mchana kweupe.
Wafanyabiashara hao licha kutoa mishahara duni tena
isiyozingatia wakati, wamekuwa wakikwepa
kukusanya michango ya wafanyakazi wao na kuiwasilisha kwenye mifuko ya hifadhi
ya jamii kama sheria inavyoelekeza.
Hali hiyo imewafanya wafanyakazi wengi kwenye sekta binafsi kuendelea
kuwa "manamba" wasio kuwa na uhakika wa kesho itakuwaje kwa makato ya kipato chao
kutowekwa kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii.
Aidha wafanyabiashara wamediliki kukiuka sheria kwa kutohakikisha
usalama wa wafanyakazi sehemu za kazi, kutowaandikisha kwenye mifuko ya hifadhi
ya jamii, kutowaruhusu kujiunga na vyama vya wafanyakazi, hawatoi likizo za
kawaida na hata za uzazi.
Kasoro nyingine za wazi ambazo zinakumbatiwa na wafanyabiashara
hao ni kutolipa malipo ya ziada,wafanyakazi kutokuwa na siku ya kupumzika na
kufanya kazi saa nyingi zaidi pasipo makubaliano ya aina yoyote.
Kwa mazingira hayo Dkt. Magufuli anapaswa kuleta mabadiliko
chanya kwa kuwafanya wafanyabiashara hao kutimiza matakwa ya kisheria kwa
wafanyakazi wao ili maisha yao yaendane na ukuaji wa pato la taifa.
Dkt. Magufuli amekuja na kauli mbiu ya "kutumbua
majipu" ambayo yameota na kumea mahali ambapo hayakustahili kuwepo
endapo uwajibikaji ungezingatiwa ipasavyo na serikali zilizotangulia.
No comments:
Post a Comment