Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Thursday, February 11, 2016

WATOTO WA MJINI, TABORA FC WAWAPOTEZA MABOYA WABISHI WA MJINI SABASABA FC KWA GOLI 3 KWA 1



Na Ramadhan Faraji, Tabora.

Ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa wa Tabora imeanza kutimua vumbi  katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi Jumatano jioni watoto wa mjini, Tabora FC  walikutana uso kwa uso na wabishi wa mjini, Saba saba FC.

Mechi hiyo ilikuwa na ushindani wa hali ya juu na  kuvuta hisia za mashabiki wengi wa Soka mjini Tabora ilimalizika kwa watoto wa mjini, Tabora FC kuwatambia wabishi wa mjini kwa kuwalaza kwa bao 3 kwa 1.

Iliwachukua dakika 4 za mchezo Saba Saba FC kumlazimisha mwamuzi wa kati wa mechi hiyo Rajabu Hussein kutoa ishara ya mpira uwekwe kati baada ya Mashaka Juma kupiga shuti kali nje ya penati box na kuiandikia timu yake bao la kwanza lilidumu kwa dakika 36.

Tabora FC walipata bao la kusawazisha kupitia kwa mchezaji wao Ajubi baada ya kuunganisha kwa kichwa mpira wa krosi na kumuacha golikipa wa Saba Saba FC Kilanga Mavumbi akigaa gaa asijue la kufanya.

Hadi timu hizo zinakwenda mapumziko zilikuwa zimefungana bao 1 kwa 1, kupindi cha pili kilianza kwa kasi huku washambuliaji wa timu zote wakijituma kupata magoli ya ushindi kwa timu zao.

Kunako dakika ya 51 mchezaji wa Tabora FC Ajubi akaifungia timu yake bao la pili, na katika dakika ya 69 Kabete akawainua tena mashabiki wa Tabora FC kwa kupachika  bao la tatu .

Dakika 90 zilimalizika na ubao wa matokeo kusomeka Tabora FC 3 na Saba Saba FC 1.

Kikosi cha Tabora FC kinanolewa na kocha Andrew Zoma na Saba Saba FC inafundishwa na kocha Mohamed Mdoma.

No comments: