Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Tuesday, February 9, 2016

SALIM KIKEKE AMPA SHAVU MSANII WA TABORA "MABOKELA"



SALIM KIKEKE
Na Deogratius Yagomba, Tabora

Msanii wa kizazi kipya mkoani Tabora Haruna J. Mabokela maarufu kama  "Mabokela" amesaini mkataba wa miaka mitatu na meneja wake mpya Abubakar Ally maarufu kwa jina la “Beka T the Boss.”

Akizungumza na Tabora Watch ilipomtembelea ofisini kwake  Mabokela amesema anaimani muziki wake sasa utafika mbali kwa kupata mkataba na meneja anayejua kazi ya muziki. 

Msanii huyo amebainisha kuwa hatua hiyo itamsogeza karibu zaidi na mashabiki wake ambao wamekuwa wakimkubali kwa kazi zake na namna anavyomiliki jukwaa kwenye “Live Show.”

Mabokela licha ya kuvipongeza vyombo vya habari kumtangaza na kucheza kazi zake amevilaumu baadhi ya vyombo hivyo kutotoa ushirikiano wa kutosha kwa wasanii wanaoibukia kwa visingizio mbalimbali ikiwemo ubora wa kazi.

Msanii huyo wa muziki wa kizazi kipya  ameweka wazi  kuwa lengo lake kubwa ni kuhakikisha muziki wake unatambulika katika mipaka ya Tanzania na kisha kuvuka nje mipaka hiyo kwa kuwa uwezo wa kufanya hivyo anao.

Ameomba wadau kuendelea kumuunga mkono kwa kuwa amekwisha andaa nyimbo mpya zikiwa kwenye hatua ya mwisho za matayarisho ya video zake na zitakapokamilika zitasambazwa kwenye vituo mbalimbali vya redio na television.

Katika hatua nyingine Mabokela amefurahishwa kuono mtangazaji wa BBC Salim Kikeke kupost wimbo wake unaojulikana kama 'SIZE YAKO kwenye mitandao ya kijamii ili wadau wamsikilize.

Amesema hatua hiyo imempa imani kubwa kuwa kazi anayo ifanya watu wanamuelewa.

Mabokela ametamba na vibao vingi kama Azizi,Maisha Hadohado,Niambie  , Size yako na vingine vingi.

No comments: