![]() |
J. F. KENNEDY |
Kazi hiyo ya kutumbua “MAJIPU” inamtengenezea maadui wenye nguvu ya fedha na ushawishi, ni vyema tahadhari za kimsingi za kiusalama zikachukuliwa.
Bokilo alitoa mfano wa Rais wa 35 wa Marekani J.F.Kennedy aliyeuawa mwaka 1963.
"Wazo
hilo la Kizalendo limenifanya nipitie historia ya Dunia kubaini namna baadhi ya
WAKUU WA NCHI walivyouawa kwa hila wakiwa madarakani wakiwahudumia wananchi wao."
BAADHI YA WAKUU WA NCHI WALIOUAWA
WAKIWA MADARAKANI KATI YA MWAKA 1865 NA MWAKA 2011:
#
|
JINA LA MKUU WA NCHI
|
SIKU YA KUUAWA AU
SHAMBULIO
|
AINA YA MAUAJI AU MUUAJI
|
1.
|
14 Aprili, 1865
|
Rais wa 16 wa Marekani
alipigwa risasi kichwani na John Wilkes Booth alipokuwa akiangalia mchezo wa
kuigiza na alifariki siku iliyofuata tarehe15 Aprili,1865. Muuaji John Wilkes
Booth alifanyikiwa kutoroka lakini baadae alipigwa risasi na kufa.
|
|
2.
|
2 Julai, 1881.
|
Rais wa 20 wa Marekani alipigwa
risasi na Charles J. Guiteau, lakini Rais huyo aliweza kuishi hadi tarehe 19
Septemba ambapo alifariki kwa sumu kwenye mzunguko wa damu yake. Charles J. Guiteau alishitakiwa kwa
mauaji na baadae kuhukumiwa kunyongwa
tarehe 30 Juni, 1882.
|
|
3.
|
6 Septemba,
1901
|
Rais wa 25 wa Marekani alipigwa
risasi mara mbili na Leon Czolgosz wakati akitembelea maonyesho ya Pan-American
yaliandaliwa Buffalo, New York.Rais huyo alikufa tarehe 14 Septemba, 1901.Muuaji
alishitakiwa na kuhukumiwa kupigwa shot ya umeme hadi kufa tarehe 29 Oktoba, 1901.
|
|
4.
|
22 Novemba,
1963
|
Rais wa 35 wa Marekani
aliuawa kwa kupigwa risasi na Lee Harvey
Oswald,wakati akiwa kwenye msafara wake Dallas, Texas. Baadae Jack Ruby alimpiga risasi na
kumuua Oswald kabla hajafikishwa mahakamani.
|
|
5.
|
Hara Takashi
|
4 Novemba, 1921
|
Waziri mkuu wa 10 wa Japan
alichomwa kisu na Nakaoka Kon'ichi katika Station ya Tōkyō. Muuaji aliachiwa
huru miaka 13 baadae.
|
6.
|
Inukai Tsuyoshi
|
15 Mei,1932
|
Waziri mkuu wa Japan.
Alipigwa risasi na askari 11 wa jeshi la nchi hiyo akiwa kwenye makazi ya
waziri mkuu katika jiji la Tokyo.
|
7.
|
Paul Doumer
|
7 Mei,1932
|
Rais wa Ufaransa aliuawa
kwa kupigwa risasi akiwa kwenye ufunguzi wa maonyesho ya Vitabu yaliyofanyika
kwenye Hôteli ya Salomon de
Rothschild jijini Paris na wakati huo akizungumza na mwandishi wa
vitabu Claude Farrère ambapo Paul Gorguloff
alifyatua risasi kadhaa na mbili zilimpata Rais huyo chini ya fuvu la kichwa
na nyingine kwenye kwapa la kulia alianguka chini na baadae kufariki akiwa
hospitalini jijini Paris.
|
8.
|
Crown Prince Louis Rwagasore
|
13 Oktoba, 1961
|
Waziri mkuu wa pili wa
taifa la Burundi.Aliuawa akiwa anapata chakula cha usiku katika Hoteli club du lac Tanganyika katika jiji la
Bujumbura, Burundi.
|
9.
|
Sylvanus Epiphanio Olympio
|
13 Januari, 1963
|
Rais wa Togo. Usiku wa manani Rais
huyo aliamshwa na kundi la askari wa jeshi la nchi hiyo na kabla ya
mapambazuko mwili wake uligunduliwa na balozi wa Marekani nchini humo Leon
B. Poullada ukiwa umbali wa futi tatu nje ya mlango wa ubalozi wa Marekani.
|
10.
|
Pierre Ngendandumwe
|
15 Januari, 1965
|
Waziri mkuu wa Burundi
aliuawa na mkimbizi wa kitusi kutoka Rwanda baada ya kuchaguliwa kuhudumu
muhula wa pili wa wadhifa huo tarehe 7 Januari, 1965.
|
11.
|
Alhaji Sir Abubakar Tafawa Balewa
|
15 Januari, 1966
|
Waziri mkuu pekee wa
Nigeria huru alipinduliwa na kuuawa na wanajeshi,mwili wake ulipatikana kando
kando ya barabara jijini Lagos siku sita baada ya tukio hilo.
|
12.
|
François Tombalbaye
|
13 Aprili,1975
|
Rais wa Chad. Aliuawa na wanajeshi
wa nchi hiyo.
|
13.
|
Park Chung-hee
|
26 Oktoba, 1979
|
Rais wa Korea ya
Kusini aliiongoza nchi hiyo tangu mwaka 1961. Aliuawa kwa kupigwa risasi na
mkurugenzi wa shirika la kijasusi la Korea KCIA Kim Jae-gyu.
|
14.
|
Muhammad Anwar El Sadat
|
6 Oktoba, 1981
|
Rais wa Misri aliuawa na
askari wakati wa gwaride lilifanyika Cairo katika kusheherekea nchi hiyo
kuvuka upande wa pili wa mfereji wa Suez.
|
15.
|
Indira Priyadarshini Gandhi
|
31 Oktoba, 1984
|
Waziri mkuu pekee
mwanamke wa India. Aliuawa na walinzi wake wawili Satwant Singh
na Beant Singh, kwa kumpiga risasi akiwa
kwenye bustani ya makazi ya waziri mkuu yaliyopo barabara ya 1 Safdarjung ,
New Delhi.
|
16.
|
Sven Olof Joachim Palme
|
28 Februari, 1986
|
Waziri mkuu wa 26 wa
Sweden. Aliuawa akiwa anatoka kuangalia sinema akiwa na mke wake Lisbet Palme
ambapo walivamiwa na muuaji na kuwafyatulia risasi, wakati huo waziri mkuu
huyo hakuwa na ulinzi.
|
17.
|
Thomas Isidore Noël Sankara
|
15 Oktoba, 1987
|
Rais wa Burkina Faso (1983-1987).
Aliuawa kwa kupigwa risasi na kundi la askari walilokuwa na silaha katika
mapinduzi yaliyoongozwa na rafiki yake wa zamani Blaise Compaoré.
|
18.
|
21 Oktoba, 1993
|
Rais wa kwanza wa
Burundi aliyechaguliwa kidemokrasia na wa kwanza kutoka kabila wa Wahutu
aliapishwa tarehe 10 Julai, 1993. Alipinduliwa na kuuawa na jeshi la Burundi.
|
|
19.
|
Juvénal Habyarimana
|
6 Aprili, 1994
|
Rais wa Rwanda aliingia madarakani
1973.Aliuawa baada ya ndege aliyokuwa akisafiria kutunguliwa karibu na uwanja
wa ndege wa kimataifa wa Kigali katika ndege hiyo pia alikuwemo Rais wa
Burundi Cyprien Ntaryamira.
|
20.
|
Cyprien Ntaryamira
|
6 Aprili, 1994
|
Rais wa Burundi aliyeingia
madarakani tarehe 5 Februari, 1994. Aliuawa kwenye ndege pamoja na Rais wa Rwanda Juvénal
Habyarimana.
|
21.
|
Agathe Uwilingiyimana
|
7 Aprili 1994
|
Waziri mkuu wa kwanza na akiwa
mwanamke wa kwanza wa Rwanda. Alishika madaraka hayo tangu tarehe 18
Julai,1993 hadi kifo chake.Aliuawa katika mauaji ya kimbari.
|
22.
|
Yitzhak Rabin
|
4 Novemba, 1995
|
Waziri mkuu wa Tano wa
Israel. Alihudumu misimu miwili katika wadhifa huo 1974-1977 na kisha 1992 hadi kifo
chake.Aliuawa kwa kupigwa risasi tatu na Yigal Amir.Rabin
alikuwa akihudhuria mkusanyiko wa Umma katika uwanja wa wafalme wa Israel (sasa
hivi unajulikana kama Rabin Square) kwa lengo la kuunga mkono Makubaliano ya
Oslo.
|
23.
|
Laurent-Désiré Kabila
|
16 Januari, 2001
|
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Congo tangu tarehe 17 Mei, 1997 baada ya kumfurusha Mobutu Sese Seko.Aliuawa
na mmoja wa walinzi wake.
|
24.
|
João Bernardo "Nino" Vieira
|
2 Machi, 2009
|
Rais wa Guinea-Bissau
.Alihudumu nafasi hiyo kwa mihula mitatu 1980-1984,1984-1999 na 2005-2009.Aliuawa
na askari wa jeshi la nchi hiyo.
|
25.
|
Muammar Muhammad Abu Minyar al-Gaddafi
|
20 Oktoba, 2011
|
Rais wa Libya tangu mwaka 1969 hadi
2011.Aliuawa na wanamgambo wa Misratan baada ya kushindwa vita vya wenyewe
kwa wenyewe.
|
No comments:
Post a Comment