Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Thursday, February 11, 2016

MKOA WA TABORA WAANDIKISHA WATOTO 53,581 ELIMU YA AWALI


MJI WA TABORA

Na Allan Ntana, Tabora


MKOA wa Tabora umefanikiwa kuandikisha jumla ya watoto 53,581 wa kuanza elimu ya awali katika mwaka wa masomo 2016 .

Hayo yamebainishwa hivi karibuni na afisa elimu mkoa wa Tabora Juma Mhina katika kikao cha wadau wa elimu kilichoketi hivi karibuni mjini hapa kikishirikisha maofisa kutoka halmashauri zote 7 za mkoa huo.

Amesema idadi hiyo ni ya watoto imeandikishwa katika halmashauri zote za mkoa huo ambapo idadi halisi ya watoto waliotarajiwa kuandikishwa ni 74,773 wavulana wakiwa 37,581 na wasichana 37,192.

Katika makisio hayo afisa elimu huo amesema wavulana walioandikishwa ni 21,664 sawa na asilimia 57.6 na wasichana ni 21,917 sawa na asilimia 58.9 ambapo jumla ya watoto wote walioandikishwa katika wilaya zote ni 53,581 sawa na asilimia 71.6.

Amefafanua kuwa halmashauri ya Manispaa ya Tabora imefanikiwa kuvuka lengo la makisio yake ambapo watoto waliotarajiwa kuandikishwa ni 4,881 lakini walioandikishwa ni 5,099 sawa na asilimia 104.5.

Mbali na Manispaa, ametaja takwimu za makisio ya kila halmashauri na idadi halisi ya watoto walioandikishwa ikiwa kwenye mabano kama ifuatavyo Igunga 17,844 (11,675), Nzega 16,643 (7,586), Urambo 8,433 (4,517), Sikonge 6,446 (2,227), Uyui 8,206 (4,801), Kaliua 9,944 (5,758) na Nzega Mji 2,376 (1,916).

Akizungumzia zoezi la uandikishwaji watoto wa kuanza darasa la kwanza Mhina amesema Mkoa huo umefanikiwa kuandikisha jumla ya watoto 64,642 sawa na asilimia 70.6 wakati matarajio ilikuwa kuandikisha watoto 91,506.

Aidha Mhina ameipongeza halmashauri ya Manispaa Tabora kwa kufanikiwa kuvuka lengo la uandikishaji ambapo iliandikisha watoto 7,644 sawa na asilimia 110 wakati matarajio yalikuwa kuandikisha watoto 6,924.

Ametaja takwimu za watoto walioandikishwa darasa la kwanza kwa kila halmashauri idadi iliyotarajiwa ikiwa kwenye mabano kama ifuatavyo Sikonge 2,569 (5,288), Kaliua 10,522 (16,042), Uyui 10,217 (16,571), Urambo 7,301 (8,844), Manispaa 7,644 (6,924), Igunga 11,675 (17,844), Nzega 12,678 (16,898) na Nzega Mji 2,036 (2,111).

No comments: