Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Thursday, February 4, 2016

MALI,CONGO DR ZATINGA FAINALI MICHUANO YA CHAN 2016 NCHINI RWANDA







Timu ya taifa ya Mali imetinga fainali ya ubingwa wa mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za nyumbani CHAN 2016 nchini Rwanda baada ya kuifunga Ivory Coast goli 1 kwa bila kwenye nusu fainali ya michuano hiyo.

Mchezaji Yves Bissoouma wa Mali alifunga goli hilo dakika ya 88 ya mchezo baada ya Hamidou Sinayoko kuugonga mpira kwa kichwa na kumfikia mfungaji.

Katika kipindi cha kwanza mchezaji wa Ivory Coast, Essis Aka alipiga shuti likagonga nguzo ya goli la Mali na baadaye penati iliyopigwa na mchezaji wa Mali, Mamadou Coulibaly iliokolewa na golikipa wa Ivory Coast, Ali Badra Sangare.

Kwa ushindi huo Mali itakutana na Congo DR kwenye fainali itakayopigwa siku ya Jumapili Kigali nchini Rwanda.

Congo DR imefuzu kucheza fainali ya michuano ya CHAN 2016 kufuatia ushindi wa penati 5 kwa 4 dhidi ya Guinea.

Congo DR na Guinea zilimaliza dakika 90 za kawaida bila kufungana na katika muda wa nyongeza wa dakika 30 mchezaji wa Congo DR Jonathan Bolingi alipachika goli kwa timu yake.

Lakini kabla ya dakika hizo za nyongeza kukamilika Guinea kupitia kwa Sory Sankhon ilipata goli la kusawazisha, hadi mwisho wa dakika 120 Congo DR 1 na Guinea 1.

Ndipo mikwaju ya penati ikaamuliwa na Congo DR kuibuka na ushindi wa penati 5 kwa 4.

No comments: