Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Sunday, February 7, 2016

DR CONGO MABINGWA WA CHAN 2016, RWANDA



Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imenyakua ubingwa wa pili wa Michuano ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za nyumbani CHAN baada ya kuibwaga Mali kwa magoli 3 kwa 0 kwenye fainali iliyopigwa Jumapili kwenye uwanja wa Amahoro jijini Kigali nchini Rwanda.

Mchezaji wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Meshack Elia aliifungia timu yake mabao mawili kabla ya Jonathan Bolingi kupachika bao la tatu na kuizamisha jahazi ya timu ya Mali.

Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo ni nchi ya kwanza kulitwaa Kombe la CHAN mwaka 2009 lilipoanzishwa na kuchezwa katika ardhi ya Ivory Coast ambapo waliifunga Ghana kwa mabao 2 kwa 0 kwenye fainali.

Wakati huo huo Ivory Coast wameshika nafasi ya tatu katika michuano hiyo ya CHAN 2016 kufuatia ushindi wa magoli 2 kwa 1 dhidi ya Guinea katika mechi ya mapema iliyochezwa kwenye uwanja huo wa Amahoro, Kigali nchini Rwanda.

No comments: