Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Sunday, February 14, 2016

AZAM FC YAKUTANA NA KISIKI CHA COAST UNION, YASHINDWA KUIONDOA SIMBA KILELENI



SHUTI LA MIRAJI ADAM LILIPENYA NGOME YA AZAM FC
Wagosi wa Kaya timu ya Coastal Union ya Tanga wamevunja mwiko wa AZAM FC kutokupoteza mechi kwenye Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kuichapa kwa bao 1 kwa bila kwenye mechi iliyochezwa Jumapili kwenye uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Bao hilo la Coastal Union lilifungwa na beki wa kulia wa timu hiyo Miraji Adam katika dakika ya 67 ya mchezo kwa shuti la mpira wa adhabu baada ya kupokea pasi fupi kutoka kwa Adeyum Saleh Ahmed.

Adhabu hiyo ilitokana na golikipa wa AZAM FC Aishi Manula kuudaka mpira na kulala nao kwa muda mrefu akiwa anaugulia maumivu badala ya kuutoa nje na kuonyesha ishara ya kuomba msaada, mwamuzi wa kati wa mechi hiyo Vicent Mlabu kutoka Morogoro kuamuru adhabu hiyo ipigwe kuelekeo lango la AZAM FC.
Matokeo hayo yameifanya Coastal Union kufikisha pointi 16 kwa mechi 19 walizocheza na kuondoka katika nafasi ya kukalia mkia kwenye msimamo wa Ligi hiyo.
 
AZAM FC imebaki na pointi zake 42 baada ya kucheza mechi 17 na ikiwa kwenye nafasi ya tatu kwenye msimamo ikitanguliwa na Vinara Simba SC wanaoongoza ligi hiyo kwa pointi 45 kwa mechi 19 ilizocheza na nafasi ya pili ikikaliwa na Yanga SC yenye pointi 43 katika mechi 18 ilizocheza .

No comments: