Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Thursday, February 25, 2016

TAMBUA AINA YA VIKAO KWA MUJIBU WA SHERIA, VINAVYOHUSISHA NGUVU YA UMMA KATIKA KUFANYA MAAMUZI



WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS, TAMISEMI, GEORGE SIMBACHAWENE

Aina ya Vikao na Nyakati za kufanyika

NA
AINA YA KIKAO
MUDA WA KUKUTANA
1.
Mkutano wa Wakazi wa Kitongoji.
-Hutakiwa kuketi kila mwezi mara moja na wakati mwingine wowote kulingana na dharura.

-Kamati ya Kitongoji ni kwa mfululizo huo tena kabla ya Mkutano wa Wakazi wote na wakati mwingine wowote kulingana na
dharura au mahitaji.

2.
Mkutano wa Wakazi wa Mtaa.
-Hupaswa kufanyika kila baada ya miezi 2 na kisha kulingana na dharura.

-Kamati ya mtaa ni kwa mpangilio huo, kabla ya Mkutano wa Wakazi wa Mtaa.

3.
Mkutano Mkuu wa kijiji
Kila baada ya miezi 3 na pia kulingana na dharura.
4.
Halmashauri ya Kijiji
-Kila baada ya mwezi na kabla ya mikutano Mikuu ya Kijiji na wakati mwingine kulingana na dharura.
5.
Kamati za Kudumu za
Halmashauri ya Kijiji
-Kila mwezi na kabla ya Halmashauri kuketi na wakati mwingine kulingana na dharura.
6.
Kamati za huduma mbalimbali
-Kuna kamati za huduma katika Kijiji kama vile Kamati ya Shule,Kamati ya UKIMWI, Kamati ya Mradi,n.k. ambazo hupaswa
kukutana kulingana na Sheria au Mwongozo unaoanzisha kamati  hiyo.
7.
Kamati ya Maendeleo ya Kata
-Hupaswa kukutana kila baada ya miezi 3 na wakati mwingine wowote kulingana na dharura.
8.
Baraza la Mamlaka ya Mji Mdogo
-Hupaswa kukutana kila miezi 3 mara moja na kulingana na dharura.
9.
Kamati za Kudumu za Mamlaka ya Mji Mdogo
-Kila baada ya miezi 3 na kulingana na dharura isipokuwa ile kamati inayohusika na fedha ni kila mwezi.
10.
Mabaraza ya Madiwani ya Wilaya,
Mji, Manispaa na Jiji
-Kila baada ya miezi 3 na kulingana na dharura.
11.
Kamati za Huduma za Halmashauri ya Wilaya, Miji, Manispaa na Majiji
-Kila baada ya miezi 3 na kulingana na dharura isipokuwa ile inayohusika na fedha ni kila mwezi.
12.
Bodi /Kamati za huduma katika
Halmashauri
-hukutana kwa mujibu wa matakwa ya Sheria au miongozo inayoanzisha Bodi/Kamati hizo.


No comments: