Na Ramadhan Faraji, Tabora.
Kwenye
Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora Jumamosi jioni Saba Saba FC “wabishi
wa mjini” wametoa darasa la kusakata kabumbu baada ya kuichapa Maji Maji FC kwa
magoli 4 kwa 1 katika mwendelezo wa ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa wa
Tabora.
Licha
ya mechi hiyo kuanza kwa kasi kwa timu zote kushambuliana kwa zamu, mvua
iliyonyesha majira ya jioni ilitibua ladha ya utandazaji wa gozi la ng’ombe na
badala yake ikawa butua butua kwa timu zote mbili.
Iliwachukua
dakika 12 tu Maji Maji FC kuandika bao la kwanza kupitia kwa Steve
aliyeunganisha mpira wa adhabu ndogo.
Kufuatia
bao hilo Maji Maji FC iliendelea kulishambulia lango la wapinzani wao lakini
washambuliaji wake hawakuwa makini kuyatumia makosa ya yaliyofanywa na mabeki
wa Saba Saba FC,Rajabu Konge na Nahodha Rajabu Ngonya kujipatia magoli.
Saba
Saba FC “Wabishi wa mjini” walifufuka kimchezo na kunako dakika ya 38
mshambuliaji wake asiyekabika Sudi Sudi “Big” alifanyikiwa kuisawazishia timu
yake baada ya kuyatumia vyema makosa yaliyofanywa na mabeki wa Maji Maji FC.
Hadi
timu hizo zinakwenda mapumziko zilikuwa zimafungana bao1 kwa 1.
Kipindi
cha pili kilianza kwa Saba Saba FC kucheza kwa kasi huku ikiwatumia walinzi wa
kushoto na kulia kuongeza mashambulizi katika lango la Maji Maji FC.
Katika
dakika ya 51 Saba Saba FC wakafanyikiwa kupata bao la pili lililofungwa na
winga machachari Kamugisha Joseph, baada ya goli hilo ni dhahiri mpira
ulionekana wa upande mmoja ambapo Saba Saba FC waliendelea kushambulia kwa
kasi.
Mshambuliaji
mwenye misuri wa Saba Saba FC Sudi Sudi “Big” aliachia shuti kali kunako dakika
ya 72 lililomshinda mlinda mlango wa Maji Maji FC na kuandika bao la 3.
Kama
haitoshi Wabishi wa Mjini wakaonyesha Ubishi wao wa kiume pale mchezaji wake
Mashaka Juma alipomchambua golikipa wa Maji Maji FC na kuandika bao la 4 na la
ushindi kwa Saba Saba FC.
Hadi
mwamuzi wa kati anapuliza filimbi kuashiria kumalizika kwa mtanange huo Saba
Saba FC 4 na Maji Maji FC 1 na hivyo kumfanya Kocha wa Saba Saba FC Mohamed
Mdoma kutoka kitemi, kifua mbele na kumuacha mpinzani wake kocha wa Maji Maji FC
John Protus akijiuliza ni wapi alipojichanganya.
Lgi hiyo ya daraja la tatu inaendelea tena Jumapili jioni katika
uwanja huo wa Ally Hassan Mwinyi ambapo maafande wa JKT Msange watashuka dimbani
kuvaana na watoto wa mjini Tabora FC.
No comments:
Post a Comment