Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Saturday, February 20, 2016

AFISA MTENDAJI APANDISHWA KIZIMBANI KWA KUOMBA RUSHWA




Na,Thomas Murugwa,Tabora.

Afisa mtendaji wa kijiji cha Igalula wilaya ya Sikonge mkoa wa Tabora Ramadhan Athuman Msumeno amefikishwa mahakamani kujibu tuhuma za kuomba rushwa kinyume cha sheria namba 11/2007 ya TAKUKURU.

Upande wa mashitaka ukiongozwa na wakili Edson Mapala wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU umedai mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya mkoa Agatha Chigulu kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo tarehe 9 Disemba,2015.

Wakili Mapalala alisema kuwa siku hiyo afisa mtendaji huyo aliomba shilingi laki tatu (300,000/-)  toka kwa Dotto Joseph  ili asimchukulie hatua za kisheria.

Mapalala ameongeza kuwa mtuhumiwa akiwa ni mtumishi wa serikali katika halmashauri ya wilaya ya Sikonge aliomba fedha hizo ili asimchukulie hatua kutokana na tuhuma za kumuua mtu mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Regina Daud.

Mtuhumiwa amekana shitaka hilo na amepelekwa rumande baada ya kukosa wadhamini wenye sifa hadi tarehe 23 mwezi huu kesi hiyo itakapoanza usikilizwaji wa awali.

No comments: