Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Sunday, February 7, 2016

LIGI DARAJA LA KWANZA:MAAFANDE WA RHINO RANGERS WAUFYATA MBELE YA MBAO FC



Na Ramadhan Faraji, Tabora.

Ligi daraja la kwanza imeendelea Jumapili kwenye uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora ambapo Rhino Rangers waliikaribisha Mbao FC ya jijini Mwanza.

Katika kipindi cha Kwanza timu hizo zilicheza kwa kusomana na kushambuliana kwa zamu na zilimaliza dakika 45 za kipindi hicho bila kufungana.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo Mbao FC ya jijini Mwanza ilifanyikiwa kupachika magoli 2 na wenyeji Rhino Rangers wakiambulia goli 1.

Hadi dakika 90 zinakamilika Mbao FC waliibuka na ushindi wa Mabao 2 kwa 1 la Rhino Rangers.

Usukani wa Ligi hiyo kwa kundi C unaongozwa na Timu ya Polisi Tabora yenye pointi 27 sawa na Geita Gold Mine yenye pointi 27 ila zikitofautiana magoli ya kufanga na kufungwa.

Timu za kundi C ligi daraja la kwanza zimebakisha mechi moja kila timu kukamilisha mzunguko wa pili ambao utaamua timu ipi ipande daraja na kucheza ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu ujao.

Kwa vinara wa kundi hilo Polisi Tabora watakamilisha mzunguko huo kwa kuikaribisha JKT Orjolo na Geita Gold Mine itakutana na JKT Kanembwa.
Kila la heri kwa Polisi Tabora kucheza ligi kuu msimu ujao.

No comments: