Na Hastin Liumba,Uyui
Mkuu wa wilaya ya Uyui mkoani Tabora Zuhura Mustapha Ali imewataka wakazi wa wilaya hiyo kujiunga mfuko na wa afya ya Jamii (CHF) ili waweze kunufaika na matibabu kwa gharama nafuu na kwa uhakika.
Mkuu huyo wa wilaya ametoa kauli hiyo wakati wa
uzinduzi wa huduma za Mfuko wa Afya ya Jamii CHF uliofanyika katika kata ya
Mabama wilayani humo.
Amesema licha ya wilaya hiyo kufanya vizuri kwa wakazi wake kuchangia na kujiunga kwenye Mfuko huo bado iko haja ya kuendelea kuwahimiza wale ambao hawajajiunga wafanye hivyo na kisha kunufaika.
Amesema licha ya wilaya hiyo kufanya vizuri kwa wakazi wake kuchangia na kujiunga kwenye Mfuko huo bado iko haja ya kuendelea kuwahimiza wale ambao hawajajiunga wafanye hivyo na kisha kunufaika.
Zuhura amesema wilaya ya Uyui kwa sasa imefikia
asilimia 24.7 ya wakazi wake kujiunga na Mfuko huo wa Afya ya Jamii na kuifanya
kuwa wilaya ya 10 kitaifa.
Meneja wa mfuko wa taifa wa Bima ya Afya kanda ya Magharibi (NHIF)
Emmanuel Adina amesema afya ni jambo jema kwa kila mwanadamu hivyo wakazi wa wilaya ya Uyui watumie fursa hiyo kujiunga na CHF.
Aidha ametumia fursa hiyo kulipia wananchi watano kiasi ha Tsh.
5,000 kiwango kilichopangwa kwa ajili ya siku hiyo uzinduzi kwa lengo la kuwafikia wazee wasiojiweza pamoja na wajane wasio na uwezo.
Naye Meneja kiongozi na rasilimali watu wa (NHIF) toka makao makuu ya mfuko huo Grace Kalanje Lobulu amesisitiza wananchi kujiunga na mfuko huo ili kuongeza ufanisi katika utoaji huduma za afya.
Lobulu amesema suala la kuhamasisha wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii CHF iwe ni ajenda ya kudumu kwa viongozi wa wilaya hiyo.
Meneja wa mfuko wa taifa wa Bima ya Afya kanda ya Magharibi (NHIF)
Emmanuel Adina amesema afya ni jambo jema kwa kila mwanadamu hivyo wakazi wa wilaya ya Uyui watumie fursa hiyo kujiunga na CHF.
Aidha ametumia fursa hiyo kulipia wananchi watano kiasi ha Tsh.
5,000 kiwango kilichopangwa kwa ajili ya siku hiyo uzinduzi kwa lengo la kuwafikia wazee wasiojiweza pamoja na wajane wasio na uwezo.
Naye Meneja kiongozi na rasilimali watu wa (NHIF) toka makao makuu ya mfuko huo Grace Kalanje Lobulu amesisitiza wananchi kujiunga na mfuko huo ili kuongeza ufanisi katika utoaji huduma za afya.
Lobulu amesema suala la kuhamasisha wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii CHF iwe ni ajenda ya kudumu kwa viongozi wa wilaya hiyo.
No comments:
Post a Comment