Na
Allan Ntana, Igunga
HOSPITALI ya wilaya Igunga Mkoani Tabora
imelipongeza Shirika la Elizabeth Glaser Pediatric Aids Foundation (EGPAF) kwa
mchango wake mkubwa uliowezesha hospitali hiyo kuboresha huduma za afya ya
uzazi kwa baba, mama na mtoto.
Pongezi
hizo zimetolewa na Mganga Mkuu wa hospitali hiyo Dr. Fidelis Mabula
alipokuwa akitoa taarifa ya hospitali kwa Afisa Habari na Mawasiliano wa
Shirika hilo Mercy Nyanda alipotembelea hospitali hiyo.
Dr
Mabula amesema misaada mbalimbali inayotolewa na shirika hilo imewezesha kupungua kwa maambukizi mapya ya
virusi vya UKIMWI toka kwa mama mjamzito mwenye VVU kwenda kwa mtoto.
Ametaja
baadhi ya misaada iliyotolewa na EGPAF kuwa ni vifaa tiba, madawa, kuwezesha
mafunzo mbalimbali kwa watoa huduma za afya ya uzazi (RCH) katika zahanati,
vituo vya afya na hospitali ya wilaya hiyo na kutoa elimu ya namna ya kumkinga
mtoto na maambukizi mapya toka kwa mama.
Dr.
Mabula amepongeza EGPAF kwa kuanzisha miradi mingi ya Afya ya uzazi kwa mama na
mtoto katika wilaya hiyo ambayo pia inasaidia wakazi wa wilaya nyingine za
jirani.
‘Shirika
la EGPAF limetupa misaada mingi sana ambayo imetuwezesha kuboresha huduma za
afya ya uzazi kwa baba, mama na mtoto na kwa kiwango kikubwa akinamama
wajawazito na wanaonyonyesha wamekuwa na mwitikio mkubwa wa kuhudhuria kliniki.’
Amesema.
Amesema mpaka sasa hospitali hiyo inajivunia uwepo
wa vifaa vya kutosha vya huduma za RCH, PMTCT, CTC, CECAP, elimu ya kutosha kwa
watoa huduma na upimaji maambuki ya VVU ikiwemo magari ya kwenda kutembelea vituo
vya kutolea huduma hizo vijijini.
Dr
Mabula amebainisha kuwa licha ya uwepo wa changamoto kadha wa kadha ikiwemo
uelewa mdogo wa wananchi na upungufu wa watoa huduma, timu yake inafanya
kazi ya kujituma, hivyo akahimiza wananchi kuendelea kujitokeza kupima afya zao
ikiwemo wanaume pamoja na wake zao.
Naye
Mratibu wa Huduma ya Afya ya Uzazi kwa baba, mama na mtoto wa wilaya hiyo
Catherin Mushi ameeleza kuwa kuboreshwa kwa huduma za afya hospitalini hapo
kumechangia kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa huduma zote za wajawazito na dawa
kwa wanaobainika kuwa na maambukizi ya VVU.
Aidha
amesema kuwa kuboreshwa kwa huduma za RCH kumefanikiwa kupunguza vifo vya
akinamama wajawazito ikiwemo kuzuia maambukizi mapya ya VVU toka kwa mama
kwenda kwa mtoto sanjari na kuimarishwa kwa huduma za uzazi wa mpango.
No comments:
Post a Comment