Na,
Thomas Murugwa, Tabora.
Adhabu
hiyo imetolewa hivi karibuni na jaji Julius Malaba baada ya kumtia hatiani
mshitakiwa kutokana na kitendo chake cha kukubali kosa dhidi yake ikiwa ni sehemu
ya maadhimisho ya siku ya sheria nchini.
Jaji
Malaba amesema ametoa adhabu hiyo kwa kuzingatia hoja zilizowakilishwa na
wakili wa utetezi Stella Nyaki kwamba mshitakiwa hakuisumbua mahakama
kutokana na kitendo chake cha kukiri kosa hilo huku akijutia tendo alilofanya.
Wakili Nyaki aliiomba mahakama itoe adhabu ndogo
kwa mshitakiwa kwa vile katika kipindi alichokaa mahabusu amejifunza mengi
amejirekebisha, ana watoto wanne wanaomtegemea,hakuipotezea mahakama muda na
pia ni kosa la kwanza.
Katika
shauri hilo wakili wa serikali Deusdedit Rwegire aliiomba mahakama hiyo
itoe adhabu kali kwa mshitakiwa kwa kitendo chake cha kumuua mtu asiyekuwa na
hatia.
Awali wakili huyo wa serikali aliiambia mahakama
hiyo kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo desemba 24/2013 katika kijiji cha
kikungulu wilaya ya sikonge.
Wakili Rwegire alisema kuwa siku hiyo mshitakiwa
akiwa amelewa bila kukusudia alisababaisha kifo cha Mbogo Masanja kwa
kumchoma tumboni kwa kutumia fimbo na kusababisha avuje damu nyingi.
Taarifa ya daktari inaonyesha kuwa Masanja ambaye
sasa ni marehemu alifariki tarehe 30 Disemba 2013 kutokana na damu nyingi
kuvujia tumboni.
No comments:
Post a Comment