
Na Allan Ntana, Sikonge
HALMASHAURI ya wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora
imepitisha bajeti ya maendeleo ya shilingi bilioni 23.859 itakayotekelezwa
katika mwaka wa fedha wa 2016/2017.
Akisoma
taarifa ya mapendekezo ya makisio ya mapato na matumizi ya wilaya hiyo kwa
mwaka 2016/2017 kwenye kikao cha baraza la madiwani Afisa Mipango wa halmashauri
hiyo Ernest Kahabi amebainisha kuwa bajeti hiyo imezingatia vipaumbele muhimu
vya miradi ya maendeleo.
Amesema
halmashauri hiyo imeomba kuidhinishiwa kiasi hicho cha shilingi bilioni 23.859
ikiwa makisio ya mapato na matumizi ya kawaida ni kiasi cha shilingi bilioni
18.818 ambazo shiling bilioni 16.612 ni matumizi ya mishahara na shilingi bililioni
2.205 ni matumizi mengineyo.
Amebainisha
kuwa miradi ya maendeleo pekee imetengewa kiasi cha shilingi bilioni 5.041 ambapo
fedha za ndani ni shilingi bilioni 3.636 (ruzuku toka Serikali Kuu ikiwa ni sh
bil 2.126 na mapato ya ndani ya halmashauri sh bil 1.559) na fedha za nje ni shilingi
bilioni 1.355 ( kutoka Serikali Kuu ikiwa ni shilingi milioni.545.887 na asasi
zisizo za kiserikali shilingi milioni 810.110).
Kahabi
amesema mapendekezo ya bajeti hiyo yatatokana na vyanzo mbalimbali vya mapato
ikiwemo ruzuku toka Serikali Kuu kiasi cha shilingi bilioni 20.455 ambapo
matumizi ya mishahara ni sh bil 16.492 na matumizi mengineyo ni shilingi bilioni
1.290 huku miradi ya maendeleo ikitengewa shilingi bilioni 2.636.
Mapato
yatokanayo na michango ya wahisani ambao ni asasi zisizo za kiserikali alisema
wanatarajia kupata kiasi cha sh mil. 810 (milioni 604 kutoka EQUIP UK na
mililioni 205 kutoka EGPAF).
Afisa Mipango huyo ameongeza kuwa halmashauri hiyo
inatarajia kukusanya kiasi cha shilingi bililioni 2.594 kutoka katika vyanzo
vyake vya ndani ambapo matumizi ya mishahara itakuwa shilingi milioni 120 na
matumizi mengineyo shilingi milioni 915 huku miradi ya maendeleo ikitengewa shilingi
bilioni 1.559 sawa na asilima 60 ya mapato yote ya ndani.
Akielezea mapendekezo ya bajeti hiyo,
iliyowasilishwa na Afisa Mipango kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa
halmashauri hiyo Philemon Magesa, Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Peter Nzalalila
aliomba madiwani waiunge mkono kwa kuwa imegusa maeneo yote ya kimaendeleo kama
walivyopendekeza.
Ametaja baadhi ya vipaumbele vya bajeti hiyo kuwa
ni kuboresha miundombinu ya Kituo cha Afya Mazinge ili kukifanya kuwa hospitali
ya wilaya, kuimarisha miundombinu ya elimu ya msingi na sekondari kwa kujenga
vyumba vya madarasa na nyumba za walimu.
Kuboresha huduma ya maji safi na salama ikiwemo
kukamilisha miradi ya maji Kipili na bwawa la maji Igumila lililopo katika kata
ya Kitunda ikiwemo ujenzi wa Soko Kuu na stendi mpya, kuanzisha kidato cha tano
katika shule ya sekondari Kamagi na kuendeleza michezo kwa vijana.
No comments:
Post a Comment