Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Friday, February 26, 2016

MAHAKAMA KUU KANDA YA TABORA YATUPILIA MBALI SHAURI LA KUPINGA MATOKEO YA UBUNGE JIMBO LA TABORA MJINI


Na, Thomas Murugwa, Tabora.
Mahakama kuu kanda ya Tabora imetupilia mbali shauri la kupinga matokeo ya uchaguzi wa Ubunge wa jimbo la Tabora mjini lililofunguliwa na wanachama wanne wa Chama Cha Wananchi CUF na kuwataka walipe gharama  walizoingia wadaiwa.

Uamuzi huo umefikiwa na jaji Leila Mgonya baada ya kukubaliana na pingamizi la mawakili wa  wadaiwa ambao ni mbunge wa jimbo, Msimamizi wa uchaguzi na mwanasheria mkuu wa serikali kwamba walalamikaji hawakuwa na mamlaka na pia hawakuonyesha haki yao iliyovunjwa wakati wa zoezi la uchaguzi.

Jaji Mgonya katika uamuzi wake aliousoma kwa saa mbili amesema kuwa anakubaliana kwamba haki yao ya kuleta shauri hilo inatokana na kifungu namba 111 (1) cha Sheria ya uchaguzi  lakini hawakuwa na mamlaka kisheria.

“kutokana na sheria za nchi ili mtu awe na mamlaka ya kufungua shauri la kupinga matokeo kama siyo mgombea inabidi aeleze jinsi gani haki yake ilivyovunjwa na pia alivyoumizwa”  amesema jaji Mgonya.

Katika maamuzi hayo, jaji Mgonya amewataka walalamikaji ambao ni wananchama wanne wa  CUF walipe gharama walizotumia wajibu maombi wakati wa uendeshaji wa shauri hilo tangu lilipofunguliwa tarehe 25 Novemba 2015 hadi  lilipomalizika.

Wanachama hao wanne wa CUf ambao ni Jumanne Mtunda ,Johari Kasanga, Shaban Mussa na Thomas Ayengo kupitia kwa wakili wao Job Kerario waliiomba mahakama itengue matokeo ya uchaguzi uliompa ubunge Emanuel Mwakasaka wa CCM kwa madai haukuwa huru na wa haki.

Upande wa wajibu maombi ulikuwa unawakilishwa na wakili mwandamizi wa serikali Juma Masanja pamoja na Kamaliza Kayaga aliyekuwa anamwakilisha mbunge wa jimbo hilo,Emmanuel Mwakasaka.


Thursday, February 25, 2016

TAMBUA AINA YA VIKAO KWA MUJIBU WA SHERIA, VINAVYOHUSISHA NGUVU YA UMMA KATIKA KUFANYA MAAMUZI



WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS, TAMISEMI, GEORGE SIMBACHAWENE

Aina ya Vikao na Nyakati za kufanyika

NA
AINA YA KIKAO
MUDA WA KUKUTANA
1.
Mkutano wa Wakazi wa Kitongoji.
-Hutakiwa kuketi kila mwezi mara moja na wakati mwingine wowote kulingana na dharura.

-Kamati ya Kitongoji ni kwa mfululizo huo tena kabla ya Mkutano wa Wakazi wote na wakati mwingine wowote kulingana na
dharura au mahitaji.

2.
Mkutano wa Wakazi wa Mtaa.
-Hupaswa kufanyika kila baada ya miezi 2 na kisha kulingana na dharura.

-Kamati ya mtaa ni kwa mpangilio huo, kabla ya Mkutano wa Wakazi wa Mtaa.

3.
Mkutano Mkuu wa kijiji
Kila baada ya miezi 3 na pia kulingana na dharura.
4.
Halmashauri ya Kijiji
-Kila baada ya mwezi na kabla ya mikutano Mikuu ya Kijiji na wakati mwingine kulingana na dharura.
5.
Kamati za Kudumu za
Halmashauri ya Kijiji
-Kila mwezi na kabla ya Halmashauri kuketi na wakati mwingine kulingana na dharura.
6.
Kamati za huduma mbalimbali
-Kuna kamati za huduma katika Kijiji kama vile Kamati ya Shule,Kamati ya UKIMWI, Kamati ya Mradi,n.k. ambazo hupaswa
kukutana kulingana na Sheria au Mwongozo unaoanzisha kamati  hiyo.
7.
Kamati ya Maendeleo ya Kata
-Hupaswa kukutana kila baada ya miezi 3 na wakati mwingine wowote kulingana na dharura.
8.
Baraza la Mamlaka ya Mji Mdogo
-Hupaswa kukutana kila miezi 3 mara moja na kulingana na dharura.
9.
Kamati za Kudumu za Mamlaka ya Mji Mdogo
-Kila baada ya miezi 3 na kulingana na dharura isipokuwa ile kamati inayohusika na fedha ni kila mwezi.
10.
Mabaraza ya Madiwani ya Wilaya,
Mji, Manispaa na Jiji
-Kila baada ya miezi 3 na kulingana na dharura.
11.
Kamati za Huduma za Halmashauri ya Wilaya, Miji, Manispaa na Majiji
-Kila baada ya miezi 3 na kulingana na dharura isipokuwa ile inayohusika na fedha ni kila mwezi.
12.
Bodi /Kamati za huduma katika
Halmashauri
-hukutana kwa mujibu wa matakwa ya Sheria au miongozo inayoanzisha Bodi/Kamati hizo.


Wednesday, February 24, 2016

ALCARDO ILAGILA:"NIMECHOKA KUCHAFULIWA KUHUSIKA KUIFILISI WETCU"




Na Hastin Liumba,Tabora

ALIYEKUWA mwenyekiti wa bodi ya Chama Kikuu cha Ushirika wa Wakulima wa Tumbaku kanda ya Magharibi (WETCU), Alcardo Ilagila amekanusha tuhuma kuwa yeye na bodi yake wamefilisi chama hicho hali ambayo ilipelekea bodi nzima kujiuzulu .

Akiongea na waandishi wa habari mwenyekiti huyo wa zamani amesema amekuwa akichafuliwa na bodi mpya ya sasa chini ya mwenyekiti wake Mkandala Gabriel Mkandala kuwa walishindwa kusimamia sheria na kanuni za ushirika hali ambayo iliisababishia hasara WETCU.

Ilagila amesema amekuwa akipigiwa simu na kuelezwa kwamba bodi mpya imekuwa ikiichafua bodi yake ambayo ililazimika kujiuzulu tarehe 23 Machi, 2013 kwa shinikizo la kupisha uchunguzi kuhusiana na tuhuma mbalimbali.

Amesema bodi mpya imeeneza uzushi kuwa yeye na bodi ya zamani aliyokuwa akioongoza waliacha benki kiasi cha Tsh mil. 7,000,000 tu jambo ambalo si kweli.

Mwenyekiti huyo wa bodi ya zamani ya WETCU amesema hadi kufikia tarehe 31 Machi ,2013  bodi yake iliacha benki Tsh. milioni 28,546,341.56.

Ilagila amefafanua kuwa katika akaunti ya benki ya CRDB kulikuwa na Tsh. mil. 23,323,559.88, NMB Tsh 829,230.96 na NBC Tsh mil.4,393,550.72.

Aidha amefafanua kuwa katika akaunti ya  benki za CRDB bodi yake iliacha dola za kimarekani  458,038.15, NMB dola 3,062.56 na NBC dola 78,806.

Kuhusu bidhaa ghalani amesema waliacha mbolea aina ya NPK 10:18:24 mifuko 15,366 katika wilaya za Urambo,Tabora na Sikonge, CAN27% N mifuko 60 katika wilaya ya Tabora mjini na UREA46% N mifuko 8,171 katika wilaya za Tabora,Urambo na Sikonge.

Ameongeza kuwa dawa ya kuua wadudu wa tumbaku iitwayo DECIS waliacha vidonge 50,965 katika wilaya za Tabora mjini na Sikonge ambapo dawa aina ya CONFIDOR ya kutibu makonyo waliacha Pakiti 4,268.

Ilagila amebainisha kuwa dawa ya maotea waliacha lita 2,552 katika wilaya za Tabora na Sikonge pamoja na magunia mapya ya kufungia tumbaku (NEW MISSIAN CLOTHES yenye urefu wa mita 1,165,188.

Ameweka wazi kuwa kasoro zilizopo sasa bodi yake haihusiki nazo kwani wanaamini walifanya vyema katika utendaji wao na kwamba bodi mpya imepita katika wilaya za Kaliua,Urambo,Sikonge na Uyui na kuongea na viongozi wa vyama vya msingi vya ushirika ikiipaka matope bodi ya zamani.
 
Ilagila amebainisha kuwa bodi mpya imekuwa ikiwaeleza viongozi hao wa vyama hivyo kuwa bodi ya zamani  ilifanya ubadhirifu na kwamba haikusimamia vyema sheria na kanuni za ushirika na hivyo kuisababishia hasara WETCU.

Mwenyekiti wa bodi mpya ya sasa Makandala Gabriel Mkandala alipohojiwa kuhusiana na malalamiko hayo amesema hana taarifa sahihi kama wajumbe wake wanaeneza hayo na hawezi kujibu chochote kwa kuwa amelazwa kwenye hospitali ya Nkinga wilayani Igunga.

“Sitazungumzia hayo kwa sasa hadi nitakapopata ushahidi lakini mimi
binafsi sihusiki  kueneza tuhuma hizo.”Amesema Mkandala.