Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Saturday, March 26, 2016

WAJUMBE WA SERIKALI ZA VIJIJI WANUFAIKA NA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASIKINI



Na Halima Ikunji,Kaliua
Wajumbe 20 wa halmashauri za serikali za vijiji wilaya ya Kaliua mkoani Tabora ambao walikuwa wakinufaika na fedha za mpango wa kunusuru kaya masikini unaosimamiwa na TASAF awamu ya tatu wameondolewa kwenye mpango huo.

Akizungumza na waandishi wa habari afisa mtendaji wa kata ya Ichemba wilayani humo Bryson Kikabiha amesema wajumbe hao waliingia kimakosa kwenye mpango huo kwa kuwa walikuwa kwenye timu za kutambua kaya masikini.

Amebainisha kuwa hatua hiyo imesababishwa na uzembe wa makusudi uliofanywa wakati wa zoezi la kutambua kaya masikini kwa kuwa wajumbe hao wa serikali za vijiji walikuwa na dhamana hiyo.

Akizungumzia suala hilo mmoja wa wajumbe hao  Gerad Katanga amesema kuwa waliamua kuingia kwenye mpango huo wa kunusuru kaya masikini kutokana na wao kutolipwa posho kwa nyadhifa walizonazo na hivyo kuwawia vigumu kujikimu kimaisha na familia zao.

Mratibu wa TASAF awamu ya tatu wilaya ya Kaliua Sabala Rukonda amesema kuwa wajumbe hao kama wataona hawakutendewa haki wakate rufaa au wajiuzulu nyadhifa zao wafanye shughuli nyingine.

No comments: