Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Tuesday, March 22, 2016

RC TABORA AOMBWA KUINGILIA KATI MGOGORO WA ARDHI KATI YA WANANCHI NA HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

AGGREY MWANRI

Na Paul Christian,Tabora.

Wamiliki wa asili wa shamba la miti lililotumika kama shamba darasa katika miaka ya 1970 kata ya Malolo katika Manispaa ya Tabora wamemuomba mkuu wa mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri kuingilia kati mgogoro kati yao na halmashauri ya Manispaa ya Tabora ambayo imetamka kulichukua shamba hilo.

Akizungumza kwa niaba ya familia tatu zinazohusika na mgogoro huo Bi Rukia Manyama amesema mnamo tarehe 8 mwezi wa pili mwaka huu alimwandikia barua mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Manispaa hiyo akiomba kupimiwa eneo hilo lililotumiwa kama shamba darasa wakati wa kampeni ya upandaji  miti katika miaka hiyo ya 1970.

Amesema baada ya kuandika barua hiyo mkurugenzi huyo alimjibu kwa barua ya tarehe 23 mwezi wa pili mwaka huu na kusainiwa kwa niaba yake na Suzana Pinini Mizengo ambapo pasipo kufafanua zaidi alieleza kuwa eneo hilo lilitwaliwa na serikali katika miaka ya 1970.

Akitoa ushahidi wake aliyekuwa afisa misitu wa serikali wakati huo Hussein Mchemba mnamo tarehe mosi mwezi wa sita, 2015 alimwandikia barua mkurugenzi huyo akimweleza kuwa eneo hilo lililotumika kama shamba darasa liliazimwa na serikali kwa lengo la kufundishia wananchi namna ya upandaji miti na sio kweli kwamba lilitwaliwa na serikali.

Katika barua hiyo ameongeza kuwa serikali ilikubaliana na familia hizo tatu kuwa endapo miti hiyo itakua na kuvunwa ardhi hiyo itarejea kwa wamiliki wa asili ambao ni familia ya Rukia Kanyama, Rashid Kambi na Cheko Masai.

Aidha katika barua hiyo Mchemba alimkumbusha Mkurugenzi huyo kuwa ni utaratibu upi uliotumika kuitwaa ardhi hiyo wakati sheria za nchi zinamaelekezo na kwa nini usitolewe ushahidi unaothibitisha kuwa serikali ililitwaa eneo hilo kisheria .

No comments: