Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Tuesday, March 15, 2016

HUSSEIN BASHE; "NILIKUWA NA NDOTO YA KUWA MBUNGE WA NZEGA TANGU NIKIWA O-LEVEL"



HUSSEIN BASHE
MBUNGE wa jimbo la Nzega mjini mkoani Tabora, Hussein Bashe amesema alianza kuwa na ndoto za kuwa mbunge wa jimbo hilo tangu mwaka 1994 akiwa anasoma sekondari.

Bashe ametoa kauli hiyo Jumanne jioni alipokuwa akihojiwa na kituo kimoja cha Televisheni hapa nchini.

Amesema kwa mara ya kwanza alijitosa kwenye kura za maoni za Chama Cha Mapinduzi CCM mwaka 2005 ili kuwania nafasi ya kuteuliwa kugombea ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya chama hicho.

“Wagombea wenye umri mdogo wakati huo tulikuwa mimi na Hamis Kigwangalla ambapo mwenzetu Lucas Selelii alishinda na chama kumteua kugombea ubunge katika jimbo la Nzega.”amesema Bashe.

Mbunge huyo amefafanua kuwa mwaka 2010 aliingia tena katika kinyang’anyiro cha kuusaka ubunge wa jimbo hilo akiwa pamoja na Hamis Kigwangalla na Lucas Selelii pamoja na wagombea wengine ambapo yeye aliongoza kura za maoni za CCM akifuatiwa na Lucas Seleli na Hamis Kigwangalla akawa wa tatu.

“Licha ya kuongoza kura za maoni chama chetu kilimteua Hamis Kigwangalla kugombea ubunge katika jimbo la Nzega na sisi tukamuunga mkono.”Amebainisha.

Bashe amefafanua kuwa katika uchaguzi wa mwaka 2015 jimbo la Nzega liligawanywa na kutoa majimbo mawili ya Nzega mjini na Nzega vijijini.

“Nilikutana na Hamis Kigwangalla na tukaamua kuweka tofauti zetu pembeni kisha tukakubaliana mimi nigombee Nzega mjini na yeye agombee Nzega vijijini.”Amesema mbunge huyo.

No comments: