Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Monday, March 14, 2016

BODI YA WETCU LTD YASHINDWA KUJIBU HOJA ZA WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA MWAKA


TUMBAKU

 
MKUTANO MKUU WA “23” WA MWAKA WA WETCU LTD ULIOFANYIKA TAREHE 28 NA 29 MWAKA 2016 KWENYE UKUMBI WA MIKUTANO WA CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA TABORA TPSC.

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Kikuu Cha Wakulima wa Tumbaku Kanda ya Magharibi WETCU LTD ambao kimsingi ni wawakilishi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika wa wakulima wa Tumbaku (AMCOS) walijadili na kuhoji Taarifa ya Mwenyekiti wa Bodi ya WETCU LTD kuhusu utekelezaji wa shughuli za Ushirika kwa mwaka 2015/2016 katika maeneo yafuatayo:-

1)  Ununuzi wa Gari jipya aina ya ZX-V8 kwa thamani ya shilingi milioni 269,010,000/-,wakati katika Mkutano Mkuu wa 22 wa mwaka 2015 wa WETCU LTD uliofanyika tarehe 01 na 02 April,2015 ulipitisha bajeti ya shilingi milioni 40 (40,000,000/-) kwa ajili ya ununuzi wa Gari.

Hoja zilizoibuliwa na Wajumbe wa Mkutano huo:-

ü Bodi ilipata wapi mamlaka ya kutumia kiasi hicho cha fedha kununulia gari wakati wao walipitisha milioni 40.
ü Je kulikuwa na ulazima wa kununua Gari hilo wakati baadhi ya vyama vya msingi vinakabiliwa na madeni na havikopesheki.
ü Je, ni kwa nini fedha hizo (Tsh. 269,010,000/-) zisingetumika kulipa madeni ambayo WETCU LTD inadaiwa na vyama vya msingi.
ü Je, Gari hilo aina ya ZX-V8 linatija gani katika kuboresha maisha ya mkulima wa Tumbaku ambaye anakabiliwa na changamoto nyingi za kinyonyaji.
ü Ni kwa nini Bodi ya WETCU LTD isingesubiri Mkutano Mkuu wa 23 ili wanachama watathmini umuhimu wa kununua Gari hilo.
ü Taarifa ya mwenyekiti wa Bodi ya WETCU LTD imeeleza kuwa fedha zilizotumika kununulia gari zilitokana na faida ya shilingi milioni 407,738,520/- baada ya kuuza na kununua Hisa katika Soko la Hisa (DSE),Kama hali ni hiyo zile shilingi milioni 40 zilitengwa kwa ajili ya ununuzi wa Gari zilikwenda wapi na kwa idhini ya nani?
ü Kwa nini fedha hizo zisingetumika kulipa madai ya wafanyakazi wa WETCU LTD ambao walipeleka shauri lao Mahakama Kuu kitengo cha kazi.

2)  Taarifa ya mwenyekiti wa Bodi ya WETCU LTD iliwataka wajumbe wa Mkutano huo waridhie kuchangia dola za Kimarekani 1.04 kwa kila bei ya mfuko wa mbolea ya NPK, CAN na UREA ili kumalizia deni lililobaki la Shilingi milioni 556,150,524/-

Hoja zilizoibuliwa na wajumbe wa Mkutano huo:-

ü Licha ya Bodi ya WETCU LTD kufanya biashara ya kuuza na kununua Hisa na kupata faida ya shilingi milioni 407,738,520/- iliona ni muhimu kununua Gari na kufanya mambo mengine badala ya kupunguza mzigo kwa mkulima wa Tumbaku kwa makato yasiyokwisha.

3)  Taarifa ya mwenyekiti wa Bodi ya WETCU LTD imeeleza kuwa walifanikiwa kuuza hisa zao staili milioni 6 katika Soko la HISA (DSE) na Kuingiza kiasi cha shilingi bilioni 2,507,738,520/- kati ya fedha hizo kiasi cha shilingi bilioni 2,100,000,000/- zilitumika kununua idadi ya HISA stahili (Right Issue) milioni 6, na hivyo kupata faida ya shilingi milioni 407,738,520/-

Mkutano mkuu wa 22 wa mwaka 2015 ulipisha azimio la kuuza HISA milioni 6 kati ya milioni 36 zilizowekezwa na WETCU LTD katika benki ya CRDB pamoja na mchango wa dola za Kimarekani 1.04 kwa kila bei ya mfuko wa NPK, UREA na CAN.
Mauzo ya HISA yaliingiza jumla ya Shilingi bilioni 2,491,909,000/- na makusanyo ya dola ya Kimarekani kwa bei ya mfuko wa mbolea yaliingiza Shilingi 718,447,680/-

Hoja zilizoibuliwa na wajumbe wa Mkutano huo:-

ü Kama makusanyo ya dola za Kimarekani 1.04 kwa kila bei ya mfuko wa mbolea ya NPK,UREA na CAN yaliingiza shilingi milioni 718,447,680 kwa mwaka 2015, wakati deni lililobaki ni milioni 556,150,524/-, Je fedha itakayozidi kwenye makusanyo hayo kwa mwaka 2016 itakwenda wapi na kwa idhini ya nani.

4)  Mrajisi wa Vyama Vya Ushirika aliwaambia wajumbe wa Mkutano huo kuwa ofisi yake iliidhinisha ombi la WETCU LTD la kutumia faida ya mauzo na manunuzi ya HISA milioni 6 kwa ajili ya kununulia Gari aina ya ZX-V8.

Hoja zilizoibuliwa na wajumbe wa Mkutano huo:-

ü Mamlaka ya kisheria aliyonayo Mrajisi wa Vyama vya Ushirika yalitathmini mahitaji ya wanachama wa WETCU LTD ambavyo ni vyama vya msingi vya Ushirika kabla ya kutoa uamuzi huo?
ü Je Mrajisi alijiridhisha kwa kiwango gani kuwa ununuzi wa Gari hilo utakuwa na tija kwa wanachama wa WETCU LTD.
ü Je, Mrajisi alikuwa na haraka gani kuidhinisha fedha hizo zitumike kununua Gari badala ya kulipeleka suala hilo kwenye mkutano mkuu ili lijadiliwe na wanachama.
ü Je, Mrajisi kwa kitendo cha kuidhinisha Bodi ya WETCU LTD kununua Gari badala ya vipaumbele vingine ana lengo la kuimarisha Ushirika?

No comments: