Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Monday, March 28, 2016

TFF YAAGIZA CHAMA CHA SOKA MKOA WA KATAVI KUCHUNGUZA USHINDI WA MAGOLI 16 KWA 0



RAIS WA TFF JAMALI MALINZI
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeagiza Chama Cha Soka Mkoa wa Katavi (KRFA) kufanya uchunguzi wa matokeo ya timu ya Stand FC kuibuka na ushindi wa magoli 16 kwa 0 dhidi ya Kamazima wakati wa mechi ya kuamua bingwa wa mkoa wa Katavi.

Mechi hiyo ilichezwa Jumamosi ilikuwa ya kuhitimisha kumpata bingwa wa mkoa huo atakayewakilisha kwenye ligi ya mabingwa mkoa ambayo inatarajiwa kuanza hivi karibuni.

Kabla ya mchezo huo uliotoa matokeo ya kushangaza, timu ya Nyundo FC ilikuwa inaongoza kwa kuwa na pointi 21 na magoli 24 ya kufunga ambapo Stand FC ilikuwa ikihitaji kufunga magoli 13 kwa 0 ili iweze kuwa mabingwa wa mkoa huo

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TFF imeeleza kuwa kutokana na Stand FC kushinda kwa mabao 16, inaonyesha kuna dalili za kupanga matokeo, hivyo KRFA haitaruhusiwa kutangaza bingwa wa mkoa wa Katavi hadi uchunguzi utakapokamilika na TFF kujiridhisha na uchunguzi huo.

Hivi karibuni TFF ilizuia kuitangaza timu iliyopanda daraja kutoka Kundi C la Ligi Daraja la Kwanza kutokana na madai ya kuwepo kwa vitendo kama hivyo ambapo katika mechi za mwisho, Geita Gold Sport iliifunga JKT Kanembwa magoli 8-0, huku Polisi Tabora ikiifunga JKT Oljoro mabao 7-0.

No comments: