Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Wednesday, April 20, 2016

TAKUKURU YAMHOJI RAIA WA VIETNAM KWA TUHUMA ZA RUSHWA.



Na, Thomas Murugwa,Tabora.

Mkuu wa kitengo cha biashara cha kampuni ya simu za mkononi mtandao wa Hallotel  Hoang Vanch Linh (36) maarufu kwa jina la “Peter”  amekamatwa na kuhojiwa  na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa  - TAKUKURU  kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa.

Akizungumza na waandishi wa habari  kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Tabora Fidelis Kalungura amesema raia huyo  wa Vietnam alikamatwa  Aprili 08 mwaka huu baada ya maofisa wake kupewa taarifa na kisha kuweka mtego uliomnasa.

Kamanda Kalungura amesema kuwa raia huyo wa Vietnam alikamatwa akipokea rushwa ya shilingi laki tano  ikiwa ni sehemu ya malipo ya shilingi milioni 1.5 alizoomba kutoka kampuni ya ulinzi iitwayo State.

Amebainisha kuwa TAKUKURU ilipewa taarifa kuwa mkuu huyo wa kitengo cha biashara Hallotel aliomba apewe fedha hizo  toka kwenye kampuni hiyo iliyopewa kazi ya kulinda minara ya simu ili waendelee kupewa mkataba wa kazi hiyo.

Kalungura amesema kwamba  mara baada ya kukamatwa na kuhojiwa  Mvietinam huyo alikana na alipewa dhamana wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

Kamanda Kalungura amebainisha kuwa bado wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo  na endapo ikibainika kama aliomba na kupokea fedha hizo kama hongo atafikishwa mahakamani .

No comments: