Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Thursday, April 7, 2016

KATA YA BUKENE YAKUSUDIA KUMALIZA UPUNGUFU WA MADAWATI



Na Lucas Raphael,Nzega

Kata  ya Bukene wilaya ya Nzega mkoani Tabora imekusudia kumaliza tatizo la madawati katika shule za msingi na sekandari katika katani humo  kwa kuchonga madawati 500 nyenye thamani ya shilingi milioni 50.
 
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mtendaji wa kata hiyo Daniel Kapama amesema kwamba kusudio hilo lilifikiwa kwenye kamati ya maendeleo ya kata kwa kuwashirikisha na wananchi wenyewe.

Amesema kwa kila mjumbe wa kamati hiyo hatachangia dawati moja na diwani wa kata hiyo ambaye ni mwenyekiti wa kamati hiyo ya maendeleo hatachingia madawati  mawili.

Kapama amebainisha kuwa  kamati hiyo ilipendekeza kumuona afisa maliasilia ili kutoa kibali cha kuchana mbao kwa ajili ya kukamilisha zoezi hilo la madawati kabla ya Juni 30 mwaka huu.

Amesema kwamba madawati hayo yatasaidia kuondoa tatizo la kukaa chini ambalo limeongezeka baada ya kuandikishwa watoto 680 kuanza darasa la kwanza na wale wa awali ni watoto 425.

Kapama amesema  kutokana na idadi hiyo ya wanafunzi imepelekea kuongezeka kiwepo kwa upungufu wa madawati kwa baadhi ya shule katika kata hiyo.

Aidha Diwani wa kata hiyo Omary shabani Omary amesema katika maazimio yao pia wamedhamiria kujenga madarasa 4 ya shule ya msingi Bukene na jengo la utawala shule ya sekondari Bukene.
  
Amesema kwamba pia wamepanga kukamilisha ujenzi wa nyumba ya sekondari Bukene ambapo kila mjumbe wa kamati ya maendeleo ya kata atachangia mfuko  moja wa saruji na wananchi  watangia kiasi cha shilingi 4,100/=.

Omary ameeleza kwamba yeye diwani atachangia mifuko miwili ya saruji  na wafanyabiashara wataungana wawili wawili kwa ajili ya kuchangia mfuko moja wa saruji .



No comments: