Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Wednesday, April 20, 2016

MAHAKAMA YATUPILIA MBALI KESI YA KUPINGA MATOKEO YA DIWANI WA CHADEMA





NA Thomas Murugwa,Tabora.

Mahakama ya hakimu mkazi mfawidhi wa wilaya ya Tabora imetupilia mbali maombi  ya Julius Salawe wa CCM aliyetaka kutenguliwa  kwa ushindi wa udiwani wa Machibya Emmanuel  wa CHADEMA katika kata ya Ugembe wilayani Nzega.

Akisoma hukumu hiyo hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo Emanuel Ngigwana amesema mlalamikaji ameshindwa kuthibitisha pasipo shaka  maombi yake yote matano ili mahakama itengue matokeo yaliyompa ushindi mgombea huyo wa CHADEMA.

Amesema kuwa  mlalamikaji alishindwa kuleta ushahidi  wa kuunga mkono madai yake ikiwemo kujaza fomu za malalamiko  ya kupinga matokeo ya vituo husika hata kupitia kwa mawakala wake.

Hakimu huyo ameeleza kuwa  katika kesi za uchaguzi,mlalamikaji amepewa jukumu  la kuthibitisha pasipo shaka yoyote madai yake dhidi ya mlalamikiwa jambo ambalo mlalamikaji katika shauri hilo ameshindwa kufanya hivyo.

Pamoja na kutupilia mbali madai hayo mahakama ilimthibitisha Machibya
wa CHADEMA kuwa diwani halali wa kata hiyo na  imemtaka mlalamikaji huyo Julius Salawe alipe gharama za uendeshaji wa shauri hilo.

Mahakama hiyo pia  imetubilia  mbali madai ya Suleiman Denis Onesmo wa CHADEMA aliyetaka kutenguliwa kwa ushindi wa diwani wa kata ya
Silambo,Wilayani Kaliua Ibrahim Issaya Kifoka wa CCM na kumthibitisha yeye kuwa diwani halali.

Hakimu Ngigwana katika uamuzi wake uliochukua  saa mbili amesema
Mlalamikaji ameshindwa kuithibitishia mahakama pasipo shaka madai yake kwa kuleta ushahidi hafifu ulioshindwa kutengua ushindi wa Kifoka.

Akisoma uamuzi  huo hakimu Ngigwana amesema madai kuwa mlalamikiwa wa kwanza  Kifoka alipeleka kura bandia 68 katika  moja ya kituo cha kupigia kura hayakuthibitishwa na mlalamikaji kwani kura hizo bandia hazikuwasilishwa  mahakamani hapo kama kielelezo.

Hakimu huyo amesema kwa ufupi mlalamikaji hakuwa na ushahidi
wenye nguvu huku ushahidi wake ukiwa ni wa kusikia na kuelezwa na watu akiwemo wakala wake.

katika madai Kwamba mlalamikiwa alimtumia  mtoto  wake Issaya Kifoka
kumsimamia, mahakama ameona kuwa  hilo halijathibitishwa na upande wa mlalamikaji kama ni kosa kwani hata mdai  alimtumia ndugu yake Paul Dennis kuwa wakala.

Kutokana na kitendo cha mlalamikaji kushindwa kuthibisha madai yake
mahakama ilimthibitisha Ibrahim  Kifoka kuwa diwani halali wa kata ya
Silambo na kuwataka wahusika kuendelea kuishi kwa amani kwani baada ya uchaguzi maisha lazima yaendelee.



No comments: