Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Thursday, April 7, 2016

NDOA ZIFUNGWE BAADA YA VIPIMO VYA AFYA



                                            Na Paul Christian, Tabora.
Imebainika kuwa baadhi ya viongozi wa dini mkoani Tabora wamekuwa wakifungisha ndoa pasipo kuhakiki vipimo vya afya vya wanandoa husika ili kuepuka kuambukizana magonjwa mbalimbali.

Uchunguzi uliofanywa na VOT FM STEREO katika Maabara kadhaa mjini Tabora umebaini kuwa baadhi ya shughuli za ndoa zimekuwa zikifunjika katika hatua za mwisho kabla ya Ndoa kufungwa baada ya ndugu wa mmoja wa wanandoa kupata taarifa zenye utata kuhusu afya ya mmoja wa wanandoa na hivyo kulazimisha wakafanyiwe vipimo.

Akizungumzia hali hiyo mmoja wa watoa huduma za Maabara ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema wamekuwa wakipokea kesi nyingi za wachumba waliokuwa kwenye hatua ya kufunga ndoa na kulazimika kufanya vipimo vya afya kwa lengo la kuhakiki uvumi unaomuhusu mmoja wa wachumba hao.

Amesema, “tunapochukua sampuli ya damu katika mazingira hayo na kwenda kupima mara nyingi tumekuwa tukigundua kuwa mmoja wa wachumba hao anaishi na virusi vya UKIMWI hali ambayo inapelekea uchumba kuvunjika katika hatua za mwisho.”

Mtaalamu huyo amefafanua kuwa hali hiyo ya fedheha,aibu na inayosababisha upotevu wa fedha na muda inaweza kuepukwa kama watu walioko kwenye uchumba wakijenga utamaduni wa kupima afya zao mapema.

Aidha amesisitiza viongozi wa dini kuacha tabia ya kufungisha ndoa kwa mazoea na badala yake wahakikishe wahusika wamefanyiwa vipimo vya afya na kukubaliana kwa dhati hata kama mmoja wao anaishi na virusi vya UKIMWI.

Afisa huyo ameshauri madhehebu ya dini kuwahimiza waumini wao walioko kwenye uchumba wa asili kufanyiwa vipimo vya virusi vya ukimwi, ujauzito,kaswende,seli mundu (sickle cell) na homa ya Ini kwa lengo la kuepuka matatizo kwenye ndoa.


Amesema, “Baadhi ya wanawake wamekuwa wakifunga ndoa wakiwa na ujauzito usiohusiana na ndoa yenyewe, kwa maana ya ujauzito wa mwanaume mwingine jambo ambalo ni  hatari.”

Mtaalam huyo wa maabara ametoa mfano wa baadhi ya wanawake ambao wamekuwa wakifanya udanganyifu kwa waume au wachumba wao kwa kwenda maabara na mashoga zao wenye mimba ambao utoa haja ndogo kwa niaba ya hao wadanganyifu na kufanyiwa vipimo vya ujauzito.

Amesema hali hiyo ya kitapeli inaweza kukomeshwa endapo wanaume watajenga mazoea ya kwenda na wenzi wao kwenye maabara wakati wa kufanyiwa vipimo muhimu kama vya ujauzito.

No comments: