MATOKEO YA VPL
JUMAMOSI 2 APRIL,2016
|
|||
1.
|
Mbeya City
|
4-0
|
Coastal Union
|
2.
|
Mwadui
|
1-2
|
Mtibwa Sugar
|
JUMAPILI 3 APRIL,2016
|
|||
1.
|
Young African
|
V
|
Kagera Sugar
|
2.
|
V
|
||
3.
|
V
|
||
4.
|
V
|
||
5.
|
v
|
YANGA YABEBWA KWA VISINGIZIO
Hatua hiyo imefikiwa baada ya klabu ya Yanga
kulalamika kupangiwa mechi tatu ndani ya wiki moja kabla ya kuvaana na Al Ahly
ya Misri Jumamosi ijayo ya terehe 9 April,2016 kwenye kinyang’anyiro cha ligi
ya Mabingwa Afrika.
Swali la kujiuliza Madai hayo ya Klabu ya Yanga
yanamsingi wowote katika soka la kisasa linalotawaliwa na uwekezaji wa
rasilimali fedha,vifaa,watu na maarifa.
Kama kweli tunataka kuimarisha Soka la Bongo inatupasa
kuacha visingizio, hoja na mitazamo ya kisiasa mahali tunapotakiwa kuonyesha
vitendo na uwezo zaidi.
Chukua mfano huu Jumamosi April 2,2016 Barcelona na
Real Madrid zimecheza mechi yao ya ligi inayojulikana kama “El Clasico” ambapo
Real Madrid iliishinda Barcelona kwa magoli 2 kwa 1.
Kwenye Ligi ya Mabingwa barani Ulaya Jumanne April
5,2016 Barcelona itakuwa kwenye uwanja wa nyumbani Camp Nou kuikaribisha
Atletico Madrid ikiwa ni hatua ya robo fainali ya michuano hiyo.
Aidha Jumatano April 6,2016 Real Madrid itakuwa
ugenini kwenye uwanja wa “Volkswagen Arena” kuivaa VfL Wolfsburg kwenye UEFA Champions League.
Timu hizo vigogo kwenye ligi kuu ya
Hispania zitashuka Dimbani kwa mara nyingine Jumamosi ya tarehe 9 April,2016
ambapo Barcelona itasafiri hadi kwenye uwanja wa Anoeta kucheza na Real
Sociedad, wakati Real Madrid itakuwa nyumbani Santiago Bernabeu wakiikaribisha timu
ya Eibar.
Hii inamaana kuwa timu hizo za
Barcelona na Real Madrid zinashuka dimbani mara tatu ndani ya wiki moja na hatujasikia zikilalamikia ratiba au kupewa
muda wa kujiandaa na UEFA Champions League.
Utaratibu huo makini uliowekwa na watu
wenye mikakati na mtazamo wenye kuzingatia weledi wa taaluma, biashara na
uwekezaji wa hali ya juu unaonekana dhahiri kwenye ligi za Uingereza,
Ujerumani, Ufaransa, Italia na nchi nyingine zilizopiga hatua kisoka.
Kama utaratibu huo unawezekana mahali
pengine duniani na timu zinafanya vizuri ni kipi kinashindikana kwa Yanga ambayo
inanolewa na kocha wa kigeni muholanzi Hans van der Pluijm.
Yanga
pia imesheheni wachezaji wa kimataifa akiwemo Vincent Bossou (Togo) , Donald
Ngoma, Thabani Kamusoko (Zimbabwe), Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima (Rwanda),
Andrey Coutinho (Brazil) na Amis Tambwe (Burundi).
Kwangu
mimi naona tunayosafari ndefu ya kufikia mafanikio ya KWELI katika mchezo wa
soka wenye mashabiki wengi, fedha nyingi na uwekezaji mkubwa kama timu zetu zitaendelea
na siasa za kubebwa na kuonewa huruma.
No comments:
Post a Comment