Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Wednesday, April 20, 2016

MARTIN JOL ATANGAZA KIKOSI CHA AL AHLY KITAKACHOIMALIZA YANGA LEO



JOL
Meneja wa timu ya Al Ahly “Red devils” ya nchini Misri Martin Jol ametangaza kikosi cha wachezaji 11 kitakachoivaa Yanga ya Tanzania katika mechi ya marudiano ya ligi ya Mabingwa barani Afrika itakayochezwa majira ya saa 19:30 kwa saa za Misri.



Mechi hiyo ya hatua ya 16 bora itachezwa leo Jumatano kwenye uwanja wa Borg El-Arab katika mji wa Alexandria.



Meneja huyo Martin Jol ametangaza kikosi hicho kuwa na wachezaji ambao ni Sherif Ekramy;Ahmed Fathi,Rami Rabia,Ahmed Hegazy,Sabry Rahil;Hossam Ashour;Hossam Ghaly;Abdallah El-Said,Momen Zakaria,Ramadan Sobhy na Amr Gamal.



Katika mechi ya kwanza iliyochezwa jijini Dar es Salaam timu hizo zilitoka sare ya bao 1 kwa 1.



Martin Jol ni mholanzi mwenye umri wa miaka 60 ni kocha wa zamani wa ligi kuu ya Uingereza ambapo amewahi kuzinoa timu za Tottenham Hotspur na Fulham.



Kocha huyo pia amewahi kuifundisha klabu ya Ajax Amsterdam ya Uholanzi na Humburger SV ya Ujerumani.



Hans van der Pluijm ni kocha wa klabu ya Yanga ya Tanzania amezaliwa tarehe 3 Januari, 1943 katika eneo la Nieuwkuijk, nchini Uholanzi.

Amewahi kuzifundisha timu kadhaa ikiwemo FC Den Bosch na amekuwa nchini Ghana tangu mwaka 1999.


Kabla ya kujiunga na Yanga amewahi kuzifundisha timu za Medeama SC,  Berekum Chelsea ambapo kwa timu za Heart of Lions na  Ashanti Gold amezinoa kwa misimu tofauti.

No comments: