Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Wednesday, April 13, 2016

ASKARI POLISI KALIUA MKOANI TABORA AKIMBIA KUKWEPA KUSHITAKIWA




Na, Thomas Murugwa, Tabora.
 
Elisha Seif David aliyekuwa askari wa jeshi la polisi kituo kidogo cha polisi King’wangoko tarafa ya Ulyankulu wilaya ya Kaliua mkoani Tabora hajulikani haliko baada ya kupata taarifa ya kukamatwa na kushitakiwa  kwa tuhuma ya  Rushwa.
 
Elisha ni miongoni mwa askari polisi wanne ambao wanadaiwa kumbambikia mche wa bhangi Dotto Gandulenya mkazi wa kijiji cha Ilege tarafa ya Ulyankulu wilayani humo na kisha kulazimisha wapewe shilingi milioni tatu ili wamuachie huru.

Askari polisi wengine watatu waliohusika kwenye tukio hilo ambalo lililopelekea  Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa  -TAKUKURU kuingilia kati  ni John Okinda, Kabila Pius na Patrick Robert.

Taarifa kutoka ndani  ya jeshi la polisi wilaya ya Kaliua zimeeleza kuwa  askari huyo alikimbia kituo chake cha kazi baada ya kutakiwa kufika ofisi ya mkuu wa polisi wilayani humo – OCD kati kati ya mwezi uliopita.

Askari  hao waliofukuzwa kazi  tayari wamekabidhiwa mikononi mwa TAKUKURU ambayo  imewafikisha mahakamani wakikabiliwa na tuhuma mbili za kuomba na kupokea rushwa kinyume na kifungu namba 15 (1) na (2) cha sheria namba 11/2007 ya TAKUKURU.

Licha ya hakimu mkazi mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Urambo Hamis Momba kuweka masharti magumu ya dhamana Katika shauri hilo la jinai namba 78/2016 waliweza kutimiza  na wapo nje hadi aprili 27 mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

No comments: