Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Saturday, July 9, 2016

VIONGOZI WATANO WA KIJIJI WAPANDISHWA KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA UHUJUMU UCHUMIUCHUMI




 Na Thomas Murugwa,Igunga.

Viongozi watano wa  serikali ya kijiji cha Igogo wilaya ya Igunga  mkoani Tabora wamefikishwa mahakama ya Wilaya hiyo wakikabiliwa na mashitaka manne ya kuhujumu uchumi.

Viongozi hao waliopandishwa kizimbani ni mwenyekiti wa kijiji hicho Elinkaila Issa, afisa mtendaji Henry Luhende Masanja, wajumbe wa kamati ya fedha Helena Maduluma  na Boniphace Jagadi pamoja  na mtunza hazina Emanuel Simon.

Upande wa mashitaka ukiongozwa na wakili Edsoni Mapalala wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa  TAKUKURU ulidai mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya Igunga Ajali Milanzi kuwa watuhumiwa walitenda makosa hayo kati ya Oktoba 13 na Novemba 24, 2014.

Katika shitaka la kwanza ilidaiwa kuwa tarehe 13 Oktoba 2014 watuhumiwa kwa kutumia nyadhifa zao waliiba shilingi 5,100,000/- fedha za shule ya msingi Igogo.

Wakili mapalala alisema kuwa watuhumiwa kwa kutumia nyadhifa zao vibaya waliiba kiasi hicho cha fedha ambazo zilikuwa zimetolewa na serikali kwa ajili ya ujenzi wa matundu 12 ya vyoo vya shule ya msingi Igogo.

 Ilidaiwa katika shitaka la pili na wakili Mapalala kuwa tarehe 24 Novemba 2014 watuhumiwa kwa pamoja waliiba shilingi 3,120,00/- zilizokuwa  zimetolewa  kwa  ajili  ya ujenzi wa choo cha ofisi ya serikali ya kijiji hicho. 

Katika shitaka la tatu  ilidaiwa na upande wa mashitaka kuwa watuhumiwa kwa pamoja na kwa makusudi  wakiwa  viongozi wa kamati ya fedha ya serikali ya kijiji hicho walijitwalia jumla ya shilingi 8,220,000/- na kusababisha ujenzi wa matundu ya vyoo kutojengwa.

Wakili Mapalala alidai katika shitaka la nne kuwa kutokana na kitendo hicho  watuhumiwa waliisababishia halmashauri ya wilaya ya Igunga hasara ya shilingi 8,220,000/=.

Watuhumiwa wote wamekana mashitaka hayo na wapo nje kwa dhamana hadi julai 12 mwaka huu shauri hilo litakapoanza usikilizwaji wa awali kwani upelelezi wake umekamilika.

No comments: