Na Paul Christian,Tabora.
Shirika
la ugavi wa umeme TANESCO mkoa wa Tabora limesema fomu za maombi ya
kuunganishiwa huduma ya umeme kwa wananchi zinatolewa bure kwenye ofisi za
shirika hilo ngazi ya wilaya na makao makuu ya mkoa.
Kaimu
meneja wa shirika hilo mkoa wa Tabora injinia Melkiad Msigwa ametoa kauli hiyo
kufuatia malalamiko ya wakazi wa tarafa ya Ulyankulu wilaya ya Kaliua kudai
kutozwa kati ya shilingi 30,000/- na 50,000/- na watu wanajiita mafundi wa
umeme ili kupata fomu hizo.
Malalamiko
hayo ya wananchi yametolewa hivi karibuni wakati wa ziara ya mbunge wa jimbo la
Ulyankulu John Peter Kadutu alipofanya ziara ya kikazi kukagua utekelezaji ya
mradi wa usambazaji umeme vijijini ambapo alizungumza na wananchi katika vijiji
vya Ibambo,Usigala, Makonge,Mkindo,Kaswa, Taba,Sasu na Kashishi jimboni humo.
Akijibu malalamiko hayo ya wananchi Kaimu meneja huyo wa TANESCO amebainisha
kuwa fomu hizo hazipaswi kuuzwa zinatolewa bure na kwamba akitokea mtu anafanya
ushawishi wa udanganyifu ili ajipatie fedha akamatwe na achukuliwe hatua za
kisheria.
Injia
Msigwa amewataka wananchi walioko kwenye vijiji vilivyounganishwa na mtandao wa
umeme kupitia mradi wa Usambaji umeme vijijini REA awamu ya pili kuzitumia
ofisi za TANESCO kwenye wilaya au kufika makao ya mkoa ya shirika mjini Tabora
ili kupata fomu hizo pamoja na taarifa nyingine muhimu.
Aidha
amewataka wananchi hao kuwatumia wataalamu kutoka kwenye makampuni
yaliyosajiliwa na ambayo yanatambuliwa na TANESCO katika kufanya utandazaji wa miundombinu
ya umeme kwenye nyumba na maeneo ya biashara.
Injia
Msigwa ametoa onyo kwa watu wanaotumia fursa ya umeme vijijini kujinufaisha kwa
udanganyifu kwa kufanya kazi za umeme majumbani pasipo vibali vya serikali
kwamba watachuliwa hatua.
Kaimu
meneja huyo wa TANESCO mkoa wa Tabora amewataka wananchi, viongozi wa serikali
za vijiji na kata ambazo zimepitiwa na umeme kuchukua tahadhari kwa kufika ofisi
za TANESCO kupata orodha ya makampuni ambayo yanatambuliwa kisheria, na hivyo
kuwa na sifa ya kuwahudumia watu vijijini.
No comments:
Post a Comment