Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Saturday, June 4, 2016

SARATANI YA NGOZI TISHIO KWA MAISHA YA ALBINO.



Na,Thomas Murugwa, Tabora.

Serikali ya awamu ya Tano imetakiwa za kunusuru maisha ya watu wenye ulemavu wa ngozi vinavyotokana na ugonjwa wa saratani ya ngozi.
 
Uchunguzi uliofanywa na blog hii umebaini kuwa vifo 10 vya watu wenye ulemavu wa ngozi  vimetokea kati ya Januari na Mei 2016  mkoani Tabora kutokana na ugonjwa huo kwa kukosa mafuta maalumu  yanayosaidia kupunguza mionzi ya jua kuifikia ngozi ya watu hao.

Katibu wa chama cha Maalbino mkoani Tabora Ramadhani Nassoro amesema  saratani ya ngozi imesababisha vifo hivyo na hiyo imekuwa ni  changamoto kwao kwa kuwa  inachangia kufupisha maisha ya watu wenye ulemavu wa ngozi.

Amesema kuwa watu wanye ulemavu wa ngozi wengi wao maisha yao hayazidi miaka (40) kwa kuwa wanakabiliwa na hatari ya saratani ya ngozi ambayo inatokana na kufikiwa na mionzi ya jua moja kwa moja.

Nassoro amebainisha kuwa albino wanakutana na mionzi ya jua kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kufanya kazi za kujipatia kipato kama kilimo, uchungaji,ujenzi na nyingine katika maeneo ya wazi.

Naye Juma Mosha katibu wa chama cha Albino wilaya ya Nzega mkoani Tabora ameiomba serikali ichukue jukumu la kuwapatia mafuta hayo maalumu kupitia  hospitali na vituo vya afya ili kuwanusuru na saratani ya ngozi ambayo inakatisha maisha yao kwa kiwango kikubwa.

Katibu huyo amebainisha kuwa mafuta hayo yanagharama kubwa hali ambayo albino wengi hawawezi kumudu na kwamba wakati umefika kwa serikali kuwasaidia kama ambavyo imeamua kufanya hivyo kwa wazee.

No comments: