Featured Post

KITUMBO:MAWASILIANO MADHUBUTI YA KIUTAWALA NI SIRI YA MAFANIKIO

Na Paul Christian, Tabora. Mawasiliano mazuri ya kiutawala baina ya wenyeviti na watendaji wa mitaa na wananchi ni jambo muhimu kat...

Saturday, June 4, 2016

MSTAAFU ALIA NA HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA KUSHINDWA KUMLIPA MAPUNJO YAKE



Na Mwandishi Wetu,Tabora

MSTAAFU aliyekuwa mtumishi wa halmashauri ya Manispaa Tabora Daud
Timotheo (70) amelia na uongozi halmashauri hiyo kushindwa kumlipa
haki yake kama mapunjo ya mshahara kiasi cha shilingi milioni 1.3.

Akiongea na waandishi wa habari mstaafu huyo amesema amefuatilia madai yake kwa muda mrefu bila mafanikio hali ambayo imemlazimu kueleza kilio chake hadharani ili asaidiwe kupata haki yake.

Timotheo amesema alistaafu  mwaka 2013 akiwa mhudumu idara ya afya katika halmashauri ya manispaa hiyo na kwamba amepunjwa muda wa miezi 15 kwa kulipwa mshahara pungufu.

Amebainisha kuwa hadi anastaafu mapunjo ya mshahara wake yalikuwa ni jumla ya shilingi milioni 1,392,710.00.

Anasema alikuwa analipwa mshahara wake kwa mwezi shilingi 255,050 kuanzia mwezi Januari 2009 hadi mwezi Novemba 2009.

Aidha ameongeza kuwa katika kipindi hicho  alikuwa akipokea mshahara wa shilingi  128,410.00 ukiwa ni pungufu ya mshahara halisi wa  shilingi 255,050.00

Timotheo amebainisha kuwa hata hivyo alirekebishiwa mshahara wake ambapo mwezi Disemba 2009 alianza kulipwa mshahara wake kamili wa shilingi 255,050.00 lakini mapunjo yake hadi leo hajalipwa na mwajiri wake huyo.

Amesema amechoshwa na hali hiyo ya kuzungushwa kulipwa fedha zake za mapunjo kwa kuwa inamkwamisha kufanya shughuli nyingine ya kujiongezea kipato.

Timotheo anasema amendika barua ya kulalamika ya mwezi Machi 27,mwaka 2010 na kuambatanisha vielelezo vyote (Salary Slip) ya miezi Disemba 2008,Januari 2009 na Disemba 2009.

Mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Tabora Sipola Liana akizungumzia suala hilo amesema kuwa amemuagiza mkaguzi wa ndani kuhakiki deni hilo na taratibu ziandaliwe ili haki ya mstaafu huyo zipatikane.



No comments: